Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 16 Sitting 6 Defence and National Service Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga taifa 76 2019-09-10

Name

Yussuf Haji Khamis

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Nungwi

Primary Question

MHE. YUSSUF HAJI KHAMIS Aliuliza:-

Kumekuwa na matukio ya watoto kuokota mabomu wakidhani ni vyuma chakavu na kisha kuwalipukia na kusababisha madhara makubwa ikiwemo vifo. Hivi karibuni watoto watano wamepoteza maisha na zaidi ya watoto 40 kujeruhiwa katika Shule ya Msingi Kihanga iliyopo Ngara Mkoani Kagera.

Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti na kukomesha tatizo hili?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA Alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Yussuf Haji Khamis, Mbunge wa Nungwi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo mengi duniani yanakabiliwa na changamoto ya kutapakaa kwa kwa silaha ndogo ndogo yakiwemo mabomu ya kutupwa kwa mkono. Pamoja na Tanzania kuwa ni nchi yenye amani, baadhi ya nchi zinazotuzunguka zimejikuta zikitumbukia katika vita vya wenyewe kwa wenyewe. Hali hiyo imesababisha baadhi ya wakimbizi kukimbia na silaha yakiwemo mabomu ya kutupwa kwa mkono na kuyatekeleza baada ya kujiona wapo salama au kuwauzia wahalifu jambo ambalo limechangia kuwepo kwa mabomu hayo katika baadhi ya maeneo ya Mkoa wa Kagera.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya vita vya Kagera, Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania lilitoa elimu kwa wananchi kutookota vitu vinavyong’ara, vifaa vya chuma na pindi wanapoona vitu hivyo watoe taarifa Vituo vya Polisi au kwenye Kambi za Jeshi iliyo karibu. Kwa maeneo yaliyotiliwa mashaka wananchi walipewa tahadhari ya kutolima, kutopita au kulisha mifugo. Aidha, Jeshi la Wananchi lilipeleka Wahandisi wa Medani kukagua maeneo hayo na kujiridhisha kama yapo salama kwa wananchi kuendelea na shughuli zao za kawaida. Hivyo, inashauriwa wananchi katika mkoa huo na mingine kuendelea kuchukua tahadhari wanapoona vitu vyenye asili ya chuma.