Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 15 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 121 2016-05-09

Name

Riziki Shahari Mngwali

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RIZIKI S. MNGWALI aliuliza:-
Kwa mila zetu za Kiafrika imezoeleka kuwa huduma ya ukunga kwa akinamama wajawazito wakati wa kujifungua hutolewa na wataalam wanawake:-
Je, Serikali haioni kuwa kwa kuweka Wakunga wanaume katika baadhi ya zahanati za Serikali nchini ni kuwadhalilisha akinamama wajawazito wanaojifungua katika zahanati hizo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Riziki Shahari Mngwali, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Wakunga wote nchini wanafanya kazi kwa mujibu wa Sheria ya Uuguzi na Ukunga ya mwaka 2010. Kwa mujibu wa sheria hiyo, Mkunga ana wajibu wa kutoa huduma ya kumsimamia mama mjamzito wakati wa uchungu, wakati wa kujifungua na baada ya kujifungua. Kwa mujibu wa sheria hiyo, Wakunga wote wa kike na wa kiume wanaruhusiwa kutoa huduma ya ukunga baada ya kufuzu mafunzo yao na kupata leseni ya kutoa huduma hizo kutoka katika Baraza la Uuguzi na Ukunga.
Mheshimiwa Naibu Spika, japo Sheria ya Uuguzi na Ukunga inampa mtaalam aliyefuzu masomo hayo kutoa huduma lakini kumekuwepo na changamoto kwa baadhi ya wanajamii kutokana na mila na desturi zinazotawala jamii husika. Kutokana na hali hiyo, Serikali itaendelea kuajiri wataalam wengi ili pale penye changamoto iweze kupatiwa ufumbuzi bila kuwakwaza wanajamii husika.