Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 17 Health and Social Welfare Ofisi ya Rais TAMISEMI. 142 2016-05-11

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:-
Hospitali ya Wilaya ya Tunduru inayohudumia majimbo mawili ina tatizo la gari kubebea wagonjwa ambapo gari lililopo ni moja na linaharibika mara kwa mara.
Je, ni lini Serikali itapeleka gari jipya katika Hospitali ya Wilaya ya Tunduru?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sikudhani Yassini Chikambo, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha 2016/2017, Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru imetenga shilingi milioni 141 kutokana na mapato ya ndani ili kununua gari la wagonjwa kwa ajili ya Hospitali ya Wilaya ya Tunduru. Vilevile katika mwaka huo zimeombewa shilingi milioni 300 kupitia maombi maalum ili kununua magari mawili kwa ajili ya vituo vya afya, ili kuboresha mfumo wa rufaa kwa wagonjwa. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kuwa azma ya Serikali ni kuhakikisha magari hayo yanapatikana kwa ajili ya huduma za afya.