Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Tunduru inayohudumia majimbo mawili ina tatizo la gari kubebea wagonjwa ambapo gari lililopo ni moja na linaharibika mara kwa mara. Je, ni lini Serikali itapeleka gari jipya katika Hospitali ya Wilaya ya Tunduru?

Supplementary Question 1

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naitwa Chikambo siyo Chikabo.
Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri naomba ikumbuke kwamba Wilaya ya Tunduru tumeendelea kukiamini Chama cha Mapinduzi kwa kutoa kura nyingi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali ikumbuke kwamba wakati wa ziara ya Mheshimiwa Rais Jakaya Mrisho Kikwete mwaka 2014 alitoa ahadi za kutoa magari ya ambulance katika vituo vya afya vya Nalarasi,Nakapanya na Matemanga. Kwa hali ile ile ya kuendelea kukiamini Chama cha Mapinduzi. Naomba Mheshimiwa Naibu Waziri aniambie ni lini sasa ahadi hiyo itatekelezwa? Ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba ahadi hii imetolewa na Mheshimiwa Rais aliyepita na ahadi hii ni ahadi ya Serikali na ndiyo maana nimesema katika mchakato huu sasa hivi kuna gari la wagonjwa, bajeti imetengwa kwa ajili ya kupelekwa. Umesema maeneo mbalimbali ambayo Mheshimiwa Rais mstaafu alitoa ahadi hiyo, hii ni ahadi ya Serikali na ninajua wazi katika mkoa ule kwa sababu una vipaumbele vingi sana. Siyo ahadi hiyo peke yake, Mheshimiwa Mbunge ameniambia kwamba mpaka walikuwa na ahadi ya Mkoa mpya wa Selous tunayajua hii kama Ofisi ya Rais TAMISEMI.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa sababu maeneo haya yana vipaumbele maalum naomba nikwambie kwamba ahadi ya Serikali iko palepale katika mchakato tulioondoka nao tutahakikisha kwamba ahadi ya Mheshimiwa Rais inatekeleza ili mradi wananchi wapate huduma bora.

Name

Stephen Hillary Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Tunduru inayohudumia majimbo mawili ina tatizo la gari kubebea wagonjwa ambapo gari lililopo ni moja na linaharibika mara kwa mara. Je, ni lini Serikali itapeleka gari jipya katika Hospitali ya Wilaya ya Tunduru?

Supplementary Question 2

MHE. STEPHEN H. NGONYANI: Mheshimiwa Mwenyekiti,ahsante, kwa kuwa tatizo la Tunduru huko linalingana kabisa na Korogwe Mjini. Ni lini Serikali itaifanya Hospitali ya Magunga iwe Hospitali Teule?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa Hospitali ya Korogwe Mjini, juzi nilipita pale katika ziara yangu wakati naenda Arusha nilitembelea Hospitali ile na nikaona kwamba congestion ya watu wa pale na mahitaji yake na kwamba Wilaya iko barabarani, bahati nzuri Naibu Waziri wa Afya juzi alifika pale hali kadhalika Waziri wa Afya alifika pale, naona kwamba haya yote nimeona ni kipaumbele hospitali ile kuwa Hospitali yetu ya Rufaa ya Mkoa ili mradi kufanya hivyo. Ninaamini mchakato unaohitajika ukikamilika na mahitaji yote hasa yanayotakiwa kwamba kuifanya hospitali ya Mkoa kukamilika basi nadhani Serikali haitosita kuhakikisha hospitalki ile inakuwa Hospitali ya Mkoa kwa vigezo vitakavyokamilika na kutokana na maelekezo kutoka Wizara ya Afya.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri Jafo nataka kuongezea kwenye suala la muundo na mgawanyo na set up kwa kuzingatia maeneo katika utoaji wa huduma ya afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeongea na Waziri wa Afya, tumeona liko tatizo la catchment areas namna zilivyowekwa na uwiano wa vituo vya afya, hospitali za Wilaya, hospitali za Mikoa na ziko nyingine ambazo maombi yako mengi sana wakiomba zipandishwe madaraja.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ingawa utaratibu unaanzia huko chini kuanzia kwenye Kata, kwenye Wilaya, kwa maana ya Halmashauri, hata hivyo tunaona haja ya Serikali kukaa na kufanya sensa maalum ya kuweka mfumo wa utaratibu mzuri ili tuende kwa utekelezaji ambao utastahiki. Kwa mfano, haiwezekani ukakuta catchment area ya kata karibu nne kukawa hakuna kituo cha afya, lakini kituo cha afya kimeelekea upande mmoja. (Makofi)
Kwa kuwa tuna uchache wa rasilimali lakini iko haja ya kufanya sensa hiyo ili baadaye tuje na mpango kazi maalum kwa kushirikiana na Wizara ya Afya tutakapopanga mpangilio mzuri wa vituo vya afya, Hospitali za Wilaya na Hospitali za Mikoa kulingana na mahitaji ya wananchi.