Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 2 Sitting 3 Energy and Minerals Wizara ya Nishati 41 2021-02-04

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. JOSEPH M. MKUNDI Aliuliza: -

Pamoja na kazi kubwa iliyofanywa na Serikali ya kusambaza umeme vijijini kupitia Mradi wa REA bado kuna shida kubwa katika maeneo ya vitongoji kwenye vijiji hivyo.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kuwa umeme unasogezwa kwenye maeneo ya vitongoji ambavyo havijapata huduma hiyo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI Alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati naomba kujibu swali la Mheshimiwa Joseph Michael Mkundi, Mbunge wa Ukerewe kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Nishati Vijijini (REA) inaendelea kutekeleza mradi wa kusambaza umeme katika vitongoji visivyokuwa na umeme kupitia mzunguko wa pili wa mradi jazilizi (Densification IIA) katika mikoa tisa ya Mbeya, Pwani, Tanga, Kilimanjaro, Dodoma, Singida, Tabora, Shinyanga na Mwanza kwa kupeleka umeme katika vitongoji 1,103 kwa kuunganisha umeme wateja wa awali wapatao 69,079. Gharama ya mradi ni shilingi bilioni 197. Utekelezaji wa mradi huu unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2021. Kazi hii ni endelevu inayofanyika pia kupitia Shirika la Umeme nchini (TANESCO).

Mheshimiwa Spika, ili kutimiza Azma ya Serikali ya kufikisha huduma ya umeme katika vitongoji, Serikali kupitia Mradi wa Densification IIB unaotarajiwa kuanza mwezi Aprili, 2021 utaendelea kupeleka umeme katika vitongoji vya mikoa kumi ya Arusha, Geita, Kagera, Katavi, Kigoma, Lindi, Morogoro, Njombe, Simiyu, Songwe, kwa kupeleka umeme katika vitongoji 1,686 na kuunganisha umeme wateja wa awali wapatao 95,334. Gharama ya mradi ni shilingi bilioni 230. Mradi huu unatarajiwa kukamilika mwezi Oktoba, 2022.