Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 4 Sitting 1 Water and Irrigation Wizara ya Maji 6 2021-08-31

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Primary Question

MHE. ALEXANDER P. MNYETI Aliuliza: -

Chanzo cha Maji cha Ihelele kilichopo Kijiji cha Nyanhomango kinasambaza maji katika Mikoa ya Shinyanga na Tabora: -

Je, ni lini Serikali itapeleka miundombinu ya maji kwenye Kijiji hicho pamoja na vijiji vingine vinavyozunguka chanzo hicho?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI Alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Alexander Pastory Mnyeti, Mbunge wa Misungwi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kijiji cha Nyanhomango kilichopo katika Kata ya Ilujamate, kinapata huduma ya maji katika Skimu yenye chanzo kilichopo katika Ziwa Victoria kwenye bomba la kutoka Mabale kwenda Mbarika. Skimu hiyo inazalisha lita 1,555,200 kwa siku ambapo maji yanayozalishwa yanatosheleza mahitaji ya eneo lote ikiwemo Kijiji cha Nyanhomango. Huduma ya maji inapatikana kwenye vituo 9 vya kuchotea maji na tanki moja lenye ujazo wa lita 135,000.

Mheshimiwa Spika, Kijiji cha Isesa katika Kata ya Ilujamate kinapata huduma ya maji kupitia skimu yenye chanzo cha kisima kirefu inayozalisha lita 116,000 kwa siku ukilinganisha na mahitaji ya kijiji hicho ambayo ni lita 91,100 kwa siku. Skimu hiyo ina vituo 12 vya kuchotea maji na tanki moja lenye ujazo wa lita 135,000.

Mheshimiwa Spika, katika bajeti ya mwaka 2021/2022, Serikali kupitia RUWASA inatekeleza Mradi mkubwa wa Maji Ilujamate – Buhingo utakaonufaisha vijiji 16 vilivyopo karibu na chanzo cha Ihelele. Vijiji hivyo ni Gukwa, Mbalama, Buhunda, Mwagimagi, Kifune, Gulumungu, Lukanga, Nyambiti, Busongo, Ng’hamve, Nyamayinza, Songiwe, Seeke, Buhingo, Kabale na Mwasagela.

Mheshimiwa Spika, utekelezaji wa mradi huo unatarajiwa kuanza mwezi Oktoba, 2021. Kazi zitakazofanyika ni ujenzi wa matenki matatu yenye jumla ya ujazo wa lita 850,000, ulazaji wa bomba kuu kilometa 34.4, mabomba ya usambazaji maji kilometa 35 na vituo vya kuchotea maji 25. Kukamilika kwa mradi huo kutaboresha huduma ya maji kutoka asilimia 73 za sasa hadi asilimia 88 mwaka 2023.