Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 46 Education, Science,Technology and Vocational Training, Ofisi ya Rais TAMISEMI. 391 2016-06-20

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Primary Question

MHE. HUSSEIN M. BASHE aliuliza:-
Halmashauri ya Mji wa Nzega haina shule hata moja ya kidato cha tano na sita na hivyo kuwafanya wanafunzi wengi kulazimika kwenda kusoma nje ya Mji wa Nzega; lakini Mbunge kwa jitihada zake amejenga vyumba viwili pamoja na bweni katika shule ya sekondari Bulende kwa ajili ya kidato cha tano na sita.
(a) Je, Serikali ipo tayari kuanzisha masomo kwa kidato cha tano kuanzia mwaka huu wa 2016;
(b) Je, ni lini Serikali itajenga vyumba vya madarasa ya kidato cha tano na sita katika shule ya sekondari Chief Itinginya ili angalau kuwe na shule mbili za kidato cha tano na sita?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hussein Mohamed Bashe, Mbunge wa Nzega Mjini, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa napenda kumpongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kazi nzuri ya ukarabati wa vyumba viwili vya madarasa katika shule ya Sekondari ya Bulende, na sasa anaendelea na ujenzi na hosteli, Mheshimiwa hongera sana kwa kazi hii nzuri. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kuhakikisha shule ya Sekondari ya Bulende inapata sifa ya kuwa ya kidato cha tano, Serikali imetenga shilingi milioni 50 kwa ajili ya ujenzi wa bweni katika bajeti ya mwaka 2016/2017. Ili shule iweze kusajiliwa kuwa ya kidato cha tano na sita inapaswa kuwa na miundombinu ya kutosha kama vyumba vya madarasa, mabweni, samani, bwalo la chakula, vyoo pamoja na uwepo wa walimu wa masomo husika.
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri inapaswa kuwasilisha maombi ya usajili wa shule katika Wizara ya Elimu, Sayansi na Ufundi ambao watatuma wataalam kukagua miundombinu ya shule kabla ya kutoa kibali. Mpango wa Serikali ni kuhakikisha miundombinu ya kutosha inajengwa kwa kushirikisha nguvu za wananchi katika shule ya Sekondari ya Chief Itinginya ili kukidhi na kusajili kuwa ya kidato cha tano.
Mheshimiwa Naibu Spika, Halmashauri imepanga kutenga bajeti katika mwaka wa fedha 2017/2018 kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya sekondari ya Chief Itinginya.