Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Primary Question

MHE. HUSSEIN M. BASHE aliuliza:- Halmashauri ya Mji wa Nzega haina shule hata moja ya kidato cha tano na sita na hivyo kuwafanya wanafunzi wengi kulazimika kwenda kusoma nje ya Mji wa Nzega; lakini Mbunge kwa jitihada zake amejenga vyumba viwili pamoja na bweni katika shule ya sekondari Bulende kwa ajili ya kidato cha tano na sita. (a) Je, Serikali ipo tayari kuanzisha masomo kwa kidato cha tano kuanzia mwaka huu wa 2016; (b) Je, ni lini Serikali itajenga vyumba vya madarasa ya kidato cha tano na sita katika shule ya sekondari Chief Itinginya ili angalau kuwe na shule mbili za kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 1

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri na commitment ya Serikali kutoa shilingi milioni 50 kwa ajili ya sekondari ya Bulunde na kutoa fedha kwa ajili ya sekondari ya Chief Itinginya. Nataka nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri swali dogo moja;
Kwa kuwa, jitihada za wananchi na Mbunge wa Jimbo la Nzega ni kumalizaS ya Bulunde ili tuwe na high school, na kwa kuwa, mahitaji ya fedha yaliyotengwa na Serikali kwa ajili ya shule ya Chief Itinginya hayatoweza kumaliza ujenzi wa shule ile kuwa na high school katika sekondari ya Chief ya Itinginya, mahitaji halisi ni shilingi milioni 250.
Je, Serikali iko tayari kuongeza fedha kwa ajili ya ujenzi wa sekondari ya Chief Itinginya, ili katika Halmashauri ya Mji wa Nzega tuwe na shule mbili za A-level ?
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba niseme wazi kwamba, Mheshimiwa Bashe kama nilivyosema pale mwanzo, ninajua una juhudi kubwa sana unaendelea kuifanya pale Nzega na umekuwa kila wakati ukija pale ofisini siyo kwa suala hilo tu, hata suala zima la kukuza uchumi wa maeneo yako ya vibanda pale, lengo ni kwamba mpate mapato muweze kuelekeza katika huduma za kijamii, kwa hiyo lazima tu-recognize juhudi kubwa unayoifanya.
Mheshimiwa Naibu Spika, lengo la Serikali kwa sababu mchakato wa bajeti wa mwaka huu umeshapita na bajeti ya mwakani tunaona ni jinsi gani tutafanya. Lengo ni kusukuma nguvu kuwasaidia watu wa Nzega. Ni kweli haiingii akilini eneo kama lile ambapo population ni kubwa, watoto wengi wanafaulu lakini wanakosa fursa ya kusoma.
Kwa hiyo, Serikali tutashirikiana nanyi kwa pamoja, Halmashauri na Ofisi ya Rais, TAMISEMI tutaangalia jinsi gani tutafanya kuiboresha Nzega sasa iwe na thamani hiyo ya ukuaji wake wa Mji na Mji wa kihistoria tokea enzi za madini ya almasi, basi watu waone mwisho wa siku wananchi wa Nzega waweze kunufaika.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nikuhakikishie kwamba, juhudi ya Serikali tutakaa pamoja tutajadiliana nini kinatakiwa kifanyike na katika muda gani na kuangalia resource zilizokuwepo tuweze kusukuma watu wa Nzega waweze kupata fursa ya elimu.

Name

Kangi Alphaxard Lugola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. HUSSEIN M. BASHE aliuliza:- Halmashauri ya Mji wa Nzega haina shule hata moja ya kidato cha tano na sita na hivyo kuwafanya wanafunzi wengi kulazimika kwenda kusoma nje ya Mji wa Nzega; lakini Mbunge kwa jitihada zake amejenga vyumba viwili pamoja na bweni katika shule ya sekondari Bulende kwa ajili ya kidato cha tano na sita. (a) Je, Serikali ipo tayari kuanzisha masomo kwa kidato cha tano kuanzia mwaka huu wa 2016; (b) Je, ni lini Serikali itajenga vyumba vya madarasa ya kidato cha tano na sita katika shule ya sekondari Chief Itinginya ili angalau kuwe na shule mbili za kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 2

MHE. KANGI A. N. LUGOLA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana.
Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo hili la kuanzisha shule za kidato cha tano katika nchi yetu linafanana kabisa na tatizo ambalo liko kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Bunda, Halmashauri ambayo ni kongwe.
Mheshimiwa Naibu Spika, hatuna hata high school moja kwenye hiyo Halmashauri yetu ya Wilaya ya Bunda. Wananchi katika miaka mitano tumewahamasisha, tumejenga mabweni na mabwalo lakini tumeshindwa kukamilisha kwa sababu ya fedha na Serikali tumekuwa tukiitaka itusaidie.
Je, Mheshimiwa Naibu Waziri uko tayari kuambatana na mimi na Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere ili twende kwenye Halmashauri yetu ukajionee juhudi za wananchi ili muweze kutusaidia?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kiufupi Mheshimiwa Kangi Lugola ndugu yangu nikuambie kwamba, mimi niko tayari kuambatana na wewe na Mheshimiwa Boniphace Mwita Getere ambaye ni jirani nyuma yangu hapa. Tutajitahidi tuende pamoja siyo kwa suala hilo la shule tu inawezekana tukabaini mambo mengi sana kwa ajili ya wananchi wa eneo hilo.

Name

Richard Phillip Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. HUSSEIN M. BASHE aliuliza:- Halmashauri ya Mji wa Nzega haina shule hata moja ya kidato cha tano na sita na hivyo kuwafanya wanafunzi wengi kulazimika kwenda kusoma nje ya Mji wa Nzega; lakini Mbunge kwa jitihada zake amejenga vyumba viwili pamoja na bweni katika shule ya sekondari Bulende kwa ajili ya kidato cha tano na sita. (a) Je, Serikali ipo tayari kuanzisha masomo kwa kidato cha tano kuanzia mwaka huu wa 2016; (b) Je, ni lini Serikali itajenga vyumba vya madarasa ya kidato cha tano na sita katika shule ya sekondari Chief Itinginya ili angalau kuwe na shule mbili za kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 3

MHE. RICHARD P. MBOGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.
Kwa kuwa, tatizo lililoko Halmashauri ya Nzega linafanana kabisa na Halmashauri ya Wilaya ya Nsimbo, haina Sekondari ya kidato cha tano na sita. Kwa kuwa, Serikali ilitupa ukomo wa bajeti bilioni 14 na tumeshindwa, tumekatwa fedha nyingi za maendeleo.
Je, Ofisi ya Rais TAMISEMI, iko tayari kututafutia fedha kwenye vyanzo vingine ili tuweze kujenga sekondari ya kidato cha tano na sita katika Halmashauri yetu ya Wilaya ya Nsimbo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli najua kwamba, mwaka huu kulikuwa na suala zima la ukomo wa bajeti lakini ndiyo mwaka pekee ambao bajeti yake imevuka tumeenda karibuni kutoka bajeti ya maendeleo ya asilimia 27 mpaka asilimia 40, kwa hiyo kuna kazi kubwa imefanyika.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa siwezi kusema kwamba, mwaka huu kuna fedha zingine zitaingia kwa sababu mchakato wa bajeti umeshapita. Lengo kubwa ni nini! Nina imani kwamba, katika mwaka mwingine wa fedha unaokuja hii itakuwa ni kipaumbele kwa sababu tunajua wazi kwamba, tumejenga shule nyingi za Kata vijana wengi wanafaulu. Kwa mfano, mwaka huu tuna vijana karibuni zaidi ya elfu tisini, lakini ukiangalia capacity yetu inaenda karibuni vijana zaidi ya elfu hamsini, maana yake inaonekana tuna tatizo kubwa sana la kuhakikisha tunaweka miundombinu kuwa-accommodate vijana wa form five na form six.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Richard Mbogo katika mchakato wa bajeti wa mwakani tuweze kuliangalia kwa pamoja zaidi. Hata ikiwezekana kwa sababu mambo haya tumesema kwamba, hata shule zingine za Kata ambazo ziko vizuri tunaweza tukazi-upgrade zile baadhi ya shule kuziongezea miundombinu kuweza kuwa shule za form five na form six.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwahiyo katika mwaka wa fedha unaokuja tutaangalia kwa pamoja ni jinsi gani tutatanya Nsimbo tupate high school moja kwa ajili ya vijana wetu.

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. HUSSEIN M. BASHE aliuliza:- Halmashauri ya Mji wa Nzega haina shule hata moja ya kidato cha tano na sita na hivyo kuwafanya wanafunzi wengi kulazimika kwenda kusoma nje ya Mji wa Nzega; lakini Mbunge kwa jitihada zake amejenga vyumba viwili pamoja na bweni katika shule ya sekondari Bulende kwa ajili ya kidato cha tano na sita. (a) Je, Serikali ipo tayari kuanzisha masomo kwa kidato cha tano kuanzia mwaka huu wa 2016; (b) Je, ni lini Serikali itajenga vyumba vya madarasa ya kidato cha tano na sita katika shule ya sekondari Chief Itinginya ili angalau kuwe na shule mbili za kidato cha tano na sita?

Supplementary Question 4

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Kwa kuwa, matatizo yaliyopo Nzega yanafanana kabisa na Halmashauri ya Morogoro hatuna high school hata moja katika Halmashauri yetu ya Morogoro Vijijini.
Je, Serikali ina mpango gani wa kutusaidia ambao ukizingatia juhudi za wananchi tumejitahidi tumejenga ile Sekondari ya Nelson Mandela. Je, Serikali ina mpango gani wa kutuongezea nguvu ili kuimalizie shule ile angalau Halmashauri hii iwe na shule hata moja ya sekondari?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nilifika kwa Mheshimiwa Mbunge, ukitoka pale Morogoro Mjini pale kwa mfano unatoka Ngerengere pale, ukienda mpaka kule mwisho unaenda Kidunda halafu mpaka kule mbali zaidi wananchi wanapata shida.
Mheshimiwa Naibu Spika, mfano mtoto akitoka pale maana yake changamoto yake ni kubwa. Ni vizuri zaidi tungepata shule moja ya form five pale, kwa hiyo naomba nikuambie kwa mwaka huu kwa sababu bajeti imeshapita, imani yangu ni kwamba kwa mwaka wa fedha unaokuja 2017/2018 anzeni kuweka maoteo ya bajeti zenu katika Halmashauri, then na sisi huko Ofisi ya Rais TAMISEMI tutaona hicho ni kipaumbele kikubwa ili eneo lile sasa la Mandela tuweze kupata shule ya form five na form six angalau tupate high school moja katika maeneo hayo na Wizara ya Elimu ikija ikiona kwamba, vigezo vimefikiwa basi shule ile itapandishwa kuwa ya form five na form six.
Mheshimiwa Mbunge, naomba nikupongeze kwa juhudi kubwa tutashirikiana kwa pamoja, naomba lianze hilo wazo kwenu then Ofisi ya Rais TAMISEMI katika mchakato wa bajeti itaona siyo mbaya sasa kuipa kipaumbele eneo hili kupata shule ya form five na form six kwa ajili ya vijana wetu.