Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 46 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 392 2016-06-20

Name

Willy Qulwi Qambalo

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY (K.n.y MHE. WILLY Q. QAMBALO) aliuliza:-
Pamoja na kuwa katika Kata ya Qurus zipo Ofisi ya Kituo cha TANESCO, Vijiji vingi vya Kata hiyo vikiwemo Gongali, Qurus, Qorongaida, Genda na G/ Lambo havijafikiwa na umeme na vichache vyenye umeme, kwango cha usambazaji ni kidogo sana:-
Je, ni lini Serikali itawapaia wananchi wa Kata hiyo huduma hiyo muhimu?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nishati na Madini napenda kujibu swali la Mheshimiwa Willy Qulwi Qambalo, Mbunge wa Karatu linaloulizwa kwa niaba yake na Mheshimiwa Flatei Massay Mbunge wa Mbulu Vijijini kama ifutavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, jina la Kata iliyoko Wilayani Karatu ni Qurus yenye vijiji vya Bashay, Doffa G‟Lambo, Gendaa, Gongali, Qorong‟aida na Qurus. Aidha, hakuna Ofisi ya kituo cha TANESCO katika Kata hii. Vijiji vyote 23 vilipangwa kupatiwa umeme katika mradi wa REA awamu ya II Wilaya ya vimewashiwa umeme na hivi sasa Mkandarasi Angelique International Ltd anaendelea na kazi ya kuwaunganishia umeme wateja. Utekelezaji wa mradi huu umefikia asilimia 99 na utakamilika ifikapo tarehe 30 Juni, mwaka huu. Gharama za mradi huu ni shilingi bilioni 53.24.
Mheshimiwa Naibu Spika, vijiji vilivyotajwa na Mheshimiwa Mbunge G‟lambo, Gongali, Qorong‟aida na Qurus vimewekwa kwenye mpango wa REA awamu ya III unaoanza Julai, 2016. Kazi ya kupeleka umeme katika Vijiji hivi itahusisha pia ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 33 yenye urefu wa kilomita 8, ujenzi wa njia ya umeme msongo wa kilovoti 0.4 yenye urefu wa kilomita 12, ufungaji wa transfoma 5 zenye ukubwa mbalimbali lakini pamoja na kuwaunganishia umeme wateja wa awali 236. Gharama ya kazi hii ni hsilingi milioni 740.