Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY (K.n.y MHE. WILLY Q. QAMBALO) aliuliza:- Pamoja na kuwa katika Kata ya Qurus zipo Ofisi ya Kituo cha TANESCO, Vijiji vingi vya Kata hiyo vikiwemo Gongali, Qurus, Qorongaida, Genda na G/ Lambo havijafikiwa na umeme na vichache vyenye umeme, kwango cha usambazaji ni kidogo sana:- Je, ni lini Serikali itawapaia wananchi wa Kata hiyo huduma hiyo muhimu?

Supplementary Question 1

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, asante sana.
Kwa kuwa, ni makosa ya uchapaji nashukuru amekiri kuwa Kata hii ya Qurus ipo na kwamba Kijiji hiki cha Gongali ndiko ofisi ya TANESCO ilipo. Sasa
kuna Vijiji ambavyo amevitaja hapa katika swali la msingi ambavyo vinaitwa Gendaa na Bashay;
Je, ni lini vitapata umeme?
Pia, kwa kuwa Wilaya hii ya Karatu ni pacha kabisa na jimbo la Mbulu Vijijini; Je, Vijiji vya Mbulu Vijiji ambavyo vinafanana kabisa kwa majina haya ya Gendaa ambavyo viko Mbulu Vijijini na Bashay ambavyo viko Mbulu Vijijini na Vijiji vingine vya Endara Gadati na Vijiji na Haidereri, Kantananati, Bashay, Yaeda Ampa lini vitapatiwa umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa katika Jimbo la Karatu ni vijiji vichache vimepata umeme. Lakini nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge anayeuliza swali kwa niaba ya Mheshimiwa Mbunge ambaye hayupo ni kwamba, vijiji vingi sana mbali na alivyovijata vya Qorong‟aida na vingine, ikiwemo na kijiji cha Changarawe kitapata umeme kule kwa Mheshimiwa wa Karatu.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na mambo mengine kijiji cha Kambi ya Faru kitapata umeme kijiji cha Udongo Mwekundu kitapata umeme, pamoja na Vijiji vingine vya Rositeti vitapata umeme, hilo ni katika Jimbo la Karatu.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika Jimbo lake Mheshimiwa Mbunge alivyouliza vijiji vya Mbulu ametaja Qorong‟aida, ametaja na vingine. Lakini kuna vijiji vingi ambavyo hajavitaja ni jumla ya vijiji 73 kwenye Jimbo la Mheshimiwa Mbunge havijapata umeme. Ninamshukuru sana anavyoendelea kuwahangaikia wananchi wa Mbulu, nimhakikishie tu ametaja vijiji vinne lakini bado kuna vijiji vingi ambavyo bado havijapata umeme kwenye Jimbo lako. Nikivitaja vitano tu kati ya vile 78 ambavyo havijapata ni pamoja na Masiedo haina umeme, Labei haina umeme, Mangandi haina umeme, vijiji vyote hivi vitapata umeme kwenye REA awamu ya tatu.

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY (K.n.y MHE. WILLY Q. QAMBALO) aliuliza:- Pamoja na kuwa katika Kata ya Qurus zipo Ofisi ya Kituo cha TANESCO, Vijiji vingi vya Kata hiyo vikiwemo Gongali, Qurus, Qorongaida, Genda na G/ Lambo havijafikiwa na umeme na vichache vyenye umeme, kwango cha usambazaji ni kidogo sana:- Je, ni lini Serikali itawapaia wananchi wa Kata hiyo huduma hiyo muhimu?

Supplementary Question 2

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa kutuhakikishia kuwa Karatu watapata umeme, maana Karatu ni katika Mkoa wangu. Vilevile katika Mkoa wa Arusha kuna maeneo mengi sana wana tatizo la umeme. Mfano wa Arumeru wananchi walitoa mashamba yao, wakachimba mashimo kwa ajili ya umeme wa REA, lakini mpaka sasa hivi wananchi wale wa Arumeru hawajapata umeme. Kuna malalamiko kuwa pesa zinazopangwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo hazifiki na hata zikifika hazifiki zote.
Je, Serikali itatatua vipi tatizo hilo la umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikubaliane na Mheshimiwa Katherine na nimpongeze sana, amehangaika sana hata kwenye ununuzi wa transformer tumeamua tununue hapa ndani kwa sababu ya juhudi zake, nakupongeza Mheshimiwa Catherine. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, ili kumuhakikishia tu wananchi wa Arusha watapata umeme, ni kweli kuna matatizo ya umeme Arumeru na kuna vijiji vingi sana kama vya Urojora pamoja na vingine havijapata umeme naelewa. Lakini kumhakikishia Mheshimiwa Magige kwenye Jimbo lote tumetenga bilioni 13.7 kwa ajili ya wananchi wa Arusha. Ili kuhakikisha kwamba, REA awamu III matatizo yote yanaisha. Sambamba na hilo yapo matatizo ya umeme hasa kwenye eneo la Arusha la kukatika katika kwa umeme.
Mheshimiwa Naibu Spika, sababu nilishazitaja lakini nidokeze tu, kwa sasa hivi Serikali kupitia TANESCO pamoja na wakandarasi tunaboresha sasa miundombinu ya umeme. Kuanzia leo, tumesema tatizo la low voltage tunakwenda kulikamilisha kwa sababu sasa tunasafirisha nguvu kubwa, tunasafirisha nguvu kubwa yenye kilovoti 400 kwa upande wa Arusha kutoka Dar es Salaam kupitia Chalinze kwenda Bagamoyo, kwenda Arusha mpaka Namanga, kilomita 664.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kwa upande ule tatizo la kukatika kwa umeme litakwisha kabisa, lakini juhudi nyingine pamoja tumeamua sasa kukatika kwa umeme kuna sababisha pia uharibifu wa transfomer na hii inasababisha wakati mwingine na utaratibu wa kununua transfomer kutoka nje. Sasa hivi kama mlivyokwisha kusikia tumetangaza na naendelea kusema tena, awamu inayokuja sasa na transfomer tutakuwa tumenunua hapa nchini kwa sababu TANALEC wana uwezo wa kutengeneza.
Mheshimiwa Naibu Spika, juhudi nyingine za kumaliza tatizo la kukatika kwa umeme wakati mwingine ni matatizo ya nguzo. Sasa hivi TANESCO imeunda kampuni tanzu ambayo itakuwa inatengeneza concrete pole kwa ajili ya kutengeneza nguzo hizo hapa nchini. Hivyo, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi kwamba, sasa tatizo la umeme litakwisha mara moja.

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY (K.n.y MHE. WILLY Q. QAMBALO) aliuliza:- Pamoja na kuwa katika Kata ya Qurus zipo Ofisi ya Kituo cha TANESCO, Vijiji vingi vya Kata hiyo vikiwemo Gongali, Qurus, Qorongaida, Genda na G/ Lambo havijafikiwa na umeme na vichache vyenye umeme, kwango cha usambazaji ni kidogo sana:- Je, ni lini Serikali itawapaia wananchi wa Kata hiyo huduma hiyo muhimu?

Supplementary Question 3

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona na kunipa nafasi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, Jimbo la Njombe Mjini halimo kwenye mpango wa REA limo kwenye mpango wa umeme unaoenda Songea, hiyo kazi hiyo haijaanza.
Je, ni lini kazi hiyo itaanza ili kusudi wananchi wa Njombe na wenyewe waweze kunufaika na umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa wananchi wa Njombe siyo kwamba hawatapata umeme wa REA wataendelea kupata umeme wa REA kama kawaida, lakini chanzo cha umeme kwa wananchi wa Njombe, Ludewa, Songea Mjini, Songea Vijijini, Namtumbo ni pamoja na ule umeme wa Makambako - Songea ambao ni wa Kilovoti 220.
Mheshimiwa Naibu Spika, siyo kweli kwamba Mheshimiwa Mbunge, nakushukuru kwamba kwa sababu hujaona chini, watu nguzo wanaweka chini lakini kazi imeshaanza. Kazi za awali za upembuzi yakinifu zimekamilika na taratibu za Mkandarasi za kuanza kazi zimekamilika, kufikia Januari mwaka unaokuja kazi rasmi za kutifua na kuweka nguzo zitakuwa zimeshaanza kabisa.

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. FLATEI G. MASSAY (K.n.y MHE. WILLY Q. QAMBALO) aliuliza:- Pamoja na kuwa katika Kata ya Qurus zipo Ofisi ya Kituo cha TANESCO, Vijiji vingi vya Kata hiyo vikiwemo Gongali, Qurus, Qorongaida, Genda na G/ Lambo havijafikiwa na umeme na vichache vyenye umeme, kwango cha usambazaji ni kidogo sana:- Je, ni lini Serikali itawapaia wananchi wa Kata hiyo huduma hiyo muhimu?

Supplementary Question 4

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza la nyongeza. Maeneo ya Kibiti, Ikwiriri, Bungu kumekuwa na tatizo la umeme kukatikakatika.
Je, lini Serikali itamaliza tatizo hili?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyokwishakueleza kwenye jibu langu la msingi na maelezo mengine ya nyongeza. Ni kweli kuna maeneo mengi ambayo bado umeme unakatika katika na sababu za kukatika nimezieleza. Lakini niseme tu, taratibu za kukamilika kwa kukatikakatika pamoja na matatizo mengine ya umeme tutakapokamilisha kusambaza hizi nguvu kubwa za kilovolt 400 na kilovolt 220 ambapo kazi rasmi itakamilika 2018/2019, kwa hiyo kuanzia wakati huo, maeneo ya Kibiti, maeneo ya Ikwiriri na maeneo mengine ya kule chini, tatizo la kukatika katika kwa umeme litakwisha kabisa.