Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Term | Session | Sitting | Sector | Ministry | Qn No | Date |
---|---|---|---|---|---|---|
2020-2025 | Session 3 | Sitting 30 | Water and Irrigation | Wizara ya Maji | 261 | 2021-05-18 |
Name
Omari Mohamed Kigua
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Kilindi
Primary Question
MHE. OMARI M. KIGUA aliuliza:-
Mheshimiwa Naibu Spika, je, ni lini Serikali itaanza mkakati wa kusambaza maji kutoka Mto Dibuluma kata ya Kibati Wilaya ya Mvomero na kuyasambaza katika kata ya Tunguli, Kwekivu, Masagalu na Songe Wilayani Kilindi?
Name
Maryprisca Winfred Mahundi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa niaba wa Waziri wa Maji naomba kujibu Swali la Mheshimiwa Omari Mohamed Kigua, Mbunge wa Kilindi kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali ina mpango wa muda mrefu wa kutekeleza mradi wa maji kwa kutumia chanzo cha mto Diburuma kwa lengo la kuboresha hali ya upatikanaji wa huduma ya maji kwa wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilindi. Hatua iliyofikiwa ni kufanyika kwa utafiti wa ubora na uwingi wa maji katika chanzo hicho ili kujiridhisha na kiwango cha maji kwa ajili ya kunufaisha vijiji vilivyopo kwenye kata nne (4) za Tunguli, Kwekivu, Masagalu na Songe. Utafiti huo utakamilika kabla ya mwezi Juni, 2021 na takwimu zitakazopatikana zitatumika kufanya usanifu wa kina kwa mradi huu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa sasa kata za Tunguli, Kwekivu, Masagalu na Songe zinapata huduma ya maji safi na salama kupitia visima virefu vitano (5) na visima vifupi kumi na tano kwa lengo la kuendelea kuboresha huduma ya maji katika kata hizo na Halmashauri ya Kilindi kwa ujumla, na mwaka wa fedha 2021/2022, Serikali imetenga kiasi cha Shilingi bilioni 2.14 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maji.
Copyright © Bunge Polis 2025. All Rights Reserved