Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 54 Youth, Disabled, Labor and Employment Ofisi ya Rais TAMISEMI. 462 2016-06-30

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. STANSLAUS S. MABULA (K.n.y. MARIAM N. KISANGI) aliuliza:-
Wajasiriamali katika Mkoa wa Dar es Salaam hususan Machinga na Mama Lishe wamekuwa wakisumbuliwa sana na Mgambo wa Jiji hali inayowafanya kushindwa kujitafutia riziki ya kila siku:-
Je, Serikali inawasaidiaje Wajasiriamali hao wadogo wodogo ambao hujipatia riziki zao kupitia biashara ndogo ndogo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mariam Nassoro Kisangi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inathamini sana mchango wa wafanyabiashara wadogo katika kukuza ajira na kipato. Hata hivyo, wafanyabiashara wadogo wote wanatakiwa kuendesha biashara zao katika maeneo yaliotengwa rasmi kwa ajili hiyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa wale wanaokiuka utaratibu huu, Halmashauri hulazimika kuwatumia Mgambo kwa ajili ya kuwaondoa wafanyabiashara hao na kuwaelekeza kwenda katika maeneo yaliotengwa rasmi. Aidha, katika kutekeleza wajibu huo, mgambo wanatakiwa kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na kuwatengea maeneo ya kufanyia biashara, Serikali inatekeleza mpango wa kurasimisha biashara katika mfumo usiokuwa rasmi ili kuzitambua, kuzisajili na kuongeza mchango wake katika ukuaji wa uchumi wa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kutumia fursa hii kuzikumbusha Halmashauri zote kutenga maeneo kwa ajili ya wafanyabiashara wadogo ili biashara hizo zifanyike katika maeneo rasmi ambayo itakuwa rahisi kuwatambua na kuwahudumia.
Aidha, wafanyabiashara wadogo wanashauriwa kuunganisha mitaji yao midogo na kuunda kampuni ndogo za biashara ili waweze kukopesheka katika Taasisi za fedha na hivyo kuongeza tija katika biashara hizo.