Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 19 Education, Science,Technology and Vocational Training, Ofisi ya Rais TAMISEMI. 155 2016-05-13

Name

Kiteto Zawadi Koshuma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KITETO Z. KOSHUMA aliuliza:-
Shule nyingi katika Wilaya ya Ilemela hususani shule za msingi zina upungufu mkubwa wa madawati:-
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa hakuna mwanafunzi anayekaa chini wakati wa masomo?
(b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuweka karakana kwa kila shule ya msingi katika Wilaya ya Ilemela na kutumia vijana wazawa kutengeneza madawati ili kuepuka tatizo hili sugu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kiteto Zawadi Koshuma, Mbunge wa Viti Maalum, lenye sehemu (a) na (b) kama ifuatavyo:-
(a) Mheshimiwa Naibu Spika, upungufu wa madawati kwa shule za msingi katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela ni madawati 13,080. Ili kukabiliana na upungufu huo Serikali katika bajeti ya mwaka wa fedha wa 2015/2016, imetenga jumla ya shilingi 228.5 kwa ajili ya upatikanaji wa madawati. Kati ya fedha hizo shilingi milioni 25.69 zinatokana na Mfuko wa Kuchochea Maendeleo katika Jimbo la CDCF.
Naomba kuchukua fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Ilemela kwa uamuzi wake wa kuelekeza fedha hizo katika upatikanaji wa madawati. Aidha, natumia fursa hii kuwakumbusha Wakuu wa Mikoa wote kuhakikisha agizo la Serikali la kumaliza tatizo la madawati ifikapo tarehe 30 Juni, 2016 liwe limekamilika kikamilifu.
(b) Mheshimiwa Naibu Spika, mazingira ya shule yanahitaji utulivu na usalama wa watoto katika kujisomea bila kuwa na bughudha, hivyo hatushauri karakana hizo kuanzishwa katika maeneo ya shule za msingi badala yake Halmashauri zinashauriwa kuimarisha karakana za Halmashauri chini ya Mhandisi wa Halmashauri ili kujenga uwezo wa kutengeneza madawati kwa gharama nafuu. Mfano mzuri ni Halmashauri ya Wilaya ya Mbarali ambao wametumia karakana ya Halmashauri kutengeneza madawati yote yanayohitajika. Natumia fursa hii kuwahamasisha vijana kujiunga katika vikundi vya ujasiriamali katika fani ya useremala ili waweze kukopesheka na kushiriki katika shughuli za utengenezaji wa madawati na shughuli nyingine katika Halmashauri.