Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kiteto Zawadi Koshuma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KITETO Z. KOSHUMA aliuliza:- Shule nyingi katika Wilaya ya Ilemela hususani shule za msingi zina upungufu mkubwa wa madawati:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa hakuna mwanafunzi anayekaa chini wakati wa masomo? (b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuweka karakana kwa kila shule ya msingi katika Wilaya ya Ilemela na kutumia vijana wazawa kutengeneza madawati ili kuepuka tatizo hili sugu?

Supplementary Question 1

MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kumuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa shule zilizoko pembezoni katika Wilaya ya Ilemela huwa zinasahaulika katika mgao wa madawati. Mfano wa shule hizo ambazo ziko pembezoni mwa Wilaya ya Ilemela ni Shule ya Bugogwa, Igombe, Isanzu, Kisuni, Kilabela, Kabangaja na zinginezo. Katika shule hizo ambazo ziko pembezoni wanafunzi ambao wanakaa chini ni wa kuanzia darasa la kwanza mpaka la tatu. Je, Serikali inatoa tamko gani kuwa madawati yanapokuwa yamegawiwa, kwa mfano nikiangalia hapa katika majibu yake inaonekana pesa iliyotengwa yatapatikana madawati 4,000 kwa bei ya Sh.50,000 kwa kila dawati, je, Serikali inanihakikishia vipi kwamba shule hizi za pembezoni zitapata mgao huo wa madawati?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la piliā€¦
SPIKA: Mheshimiwa umeshauliza mawili tayari.
MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nimeuliza moja. Swali la pili, je...
SPIKA: Mheshimiwa Kiteto samahani. Mheshimiwa Waziri kati ya hayo mawili utachagua moja la kujibu, haya endelea na swali la pili.
MHE. KITETO Z. KOSHUMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Je, Serikali haioni sasa kwamba ni wakati wa kuruhusu Halmashauri za Mkoa wa Mwanza kutumia msitu wa Buhindi ambao haujavunwa kwa muda mrefu sasa, miti ivunwe kwa ajili ya kutengeneza madawati ili kukidhi tatizo hili sugu la madawati katika Mkoa wa Mwanza? Nashukuru.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, Mheshimiwa Koshuma amezungumza agenda muhimu sana hapa, upelekaji wa madawati katika maeneo ya pembeni. Kwa uzoefu wangu nilipotembelea maeneo mbalimbali siyo madawati peke yake, hata Walimu tunaowapeleka katika migao mbalimbali wengi sana wanaishia maeneo ya mijini.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama mlikuwa mnafuatilia vyombo vya habari juzi juzi nimetembelea shule moja ya Manispaa ya Dodoma iliyoko pembezoni hata mgao wa madawati haufiki kule na nikatoa maelekezo sasa shule hiyo ina madawati ya kutosha. Kwa hiyo, natoa maelekezo kwa Wakurugenzi wote wa Halmashauri wahakikishe madawati yanafika maeneo ya pembezoni hasa tukizingatia kwamba shule za pembezoni huwa zinasahaulika.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika ziara zangu nitakazozifanya utaratibu wangu utakuwa uleule, sitatoa taarifa ni shule gani nakwenda kuitembelea na Mkurugenzi ambaye nitafika katika Halmashauri yake, niki-pick shule nikikuta hakuna madawati maana yake ameshindwa kukidhi vigezo na maelekezo ya Serikali za Mitaa. Kwa hiyo, naomba nitoe onyo kabisa. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, ni kuhusu kutumia msitu, kuna misitu ya vijiji na mingine ni ya Serikali Kuu. Nadhani Ofisi ya Mkuu wa Wilaya itaangalia utaratibu na kuona tunafanyaje na kama kuna uwezekano msitu huo uweze kutumika. Vilevile nizishauri Halmashauri, wakati mwingine mbao zinakamatwa badala ya kukaa mpaka zinachakaa wakati Halmashauri ina shida ya madawati, tuangalie namna ya kufanya mbao zile ziweze kutumika kwa ajili ya kuondoa tatizo la madawati katika shule zetu.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KITETO Z. KOSHUMA aliuliza:- Shule nyingi katika Wilaya ya Ilemela hususani shule za msingi zina upungufu mkubwa wa madawati:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa hakuna mwanafunzi anayekaa chini wakati wa masomo? (b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuweka karakana kwa kila shule ya msingi katika Wilaya ya Ilemela na kutumia vijana wazawa kutengeneza madawati ili kuepuka tatizo hili sugu?

Supplementary Question 2

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kunipatia nafasi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama ambavyo wote tunajua kuna tatizo kubwa sana la madawati na Halmashauri nyingi sasa hivi zinatengeneza madawati. Swali langu la msingi ni kwamba, je, ni nani anayedhibiti ubora wa madawati hayo? Kwa sababu yawezekana kabisa mbao hizo wakati mwingine zinaweza zikawa hazijakauka vizuri na maana yake ni kwamba hayo madawati hayatadumu. Swali langu ni nani anayedhibiti kuhakikisha kwamba mbao zinazotengeneza madawati hayo ni bora na zimekauka ili isiwe tunafanya kazi ya zimamoto? Nashukuru.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la quality control (ubora wa madawati) ndiyo maana Ofisi ya Rais, TAMISEMI, imegawanyika katika Halmashauri na Mikoa na huko tuna watu tunaita wahandisi au mainjinia ambao jukumu lao kubwa kwa kila kitu kinachotengenezwa sio madawati peke yake hata majengo, kuhakikisha wanazingatia viwango vya ubora ili tupate vitu katika ubora unaokusudiwa. Kwa hiyo, tuliowapa dhamana hii ni Wahandisi wa Halmashauri wetu kuhakikisha kwanza madawati hayo yanakidhi vigezo siyo kwa ajili ya uvyevunyevu peke yake hata mbao ya aina gani inatumika ili tupate madawati siyo ya kutumika mwaka mmoja bali ya muda mrefu.

Name

Edward Franz Mwalongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Njombe Mjini

Primary Question

MHE. KITETO Z. KOSHUMA aliuliza:- Shule nyingi katika Wilaya ya Ilemela hususani shule za msingi zina upungufu mkubwa wa madawati:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa hakuna mwanafunzi anayekaa chini wakati wa masomo? (b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuweka karakana kwa kila shule ya msingi katika Wilaya ya Ilemela na kutumia vijana wazawa kutengeneza madawati ili kuepuka tatizo hili sugu?

Supplementary Question 3

MHE. EDWARD F. MWALONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba nimuulize Mheshimiwa Naibu Waziri, anasema tusiweke karakana kwenye shule za msingi lakini kuna vituo vya shule za msingi ambavyo vina ufundi, watoto huwa wanachaguliwa darasa la saba wengine wanakwenda sekondari wengine ufundi na vituo hivi vipo kwenye shule za msingi na vina fani za useremala. Je, Serikali iko tayari kusaidia kituo kama cha Shule ya Msingi Uwemba ili kusudi kiweze kutengeneza madawati kwa ajili ya Jimbo la Njombe Mjini?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kuna shule zingine zina karakana na hii nadhani ni kutokana na maelekezo kwamba tuwafunze wanafunzi wetu masomo ya ufundi. Kama shule ina kiwanda cha ufundi maana yake hata kiwanda chake kimewekwa kwa minajili kwamba hakitaathiri mazingira ya shule. Miongoni mwa zile shule ambazo tutazibainisha ni shule ambazo ndani yake zina karakana. Ofisi ya Rais, TAMISEMI ni jukumu lake kubwa kuangalia shule hizi sasa zinashiriki vipi, siyo kuziwezesha peke yake, isipokuwa kuona kwamba programu hii inakuwa endelevu ili vijana watakaotoka hapo wawe na ufundi bora.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimweleze Mheshimiwa Mbunge kwamba na mimi nitatamani sana nikifika Jimboni kwake anipeleke katika shule hiyo ili kwa pamoja tubadilishane mawazo kuhusu kuisaidia shule hiyo. Lengo likiwa ni kuongeza stadi za kazi kwa wanafunzi wetu lakini kurahisisha mambo mengine ambayo yanaweza kufanyika katika Halmashauri husika yaweze kwenda vizuri.

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. KITETO Z. KOSHUMA aliuliza:- Shule nyingi katika Wilaya ya Ilemela hususani shule za msingi zina upungufu mkubwa wa madawati:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha kuwa hakuna mwanafunzi anayekaa chini wakati wa masomo? (b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kuweka karakana kwa kila shule ya msingi katika Wilaya ya Ilemela na kutumia vijana wazawa kutengeneza madawati ili kuepuka tatizo hili sugu?

Supplementary Question 4

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru. Sambamba na suala la madawati, wananchi wameitikia wito wa uandikishaji wa watoto shule za awali pamoja na darasa la kwanza. Je, Serikali iko tayari sasa kupeleka Walimu wa madarasa haya ya awali kwa sababu madarasa hayo hayana Walimu?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba tuweke rekodi sawa, katika utekelezaji wa ahadi ya Chama cha Mapinduzi na Ilani yake lakini azimio la Mheshimiwa Rais kuhakikisha watu wote wanakwenda shuleni, tumepata mafanikio makubwa sana na ni kweli tumepata ongezeko la wanafunzi na shule zingine zime-burst. Shule ambayo ilikuwa inatarajia kusajili wanafunzi 500 wamesajili mpaka wanafunzi 1,000, haya ni mafanikio makubwa katika Taifa letu hili.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mujibu wa utaratibu uliopo sasa Walimu wote wanaosoma ngazi ya certificate wanakuwa na component ya elimu ya awali. Kwa hiyo, imani yangu kubwa ni kwamba katika ajira ambazo tunatarajia kuzitoa mwaka huu ambapo siyo muda mrefu ujao, suala hilo la kuzingatia Walimu ambao watakwenda kufundisha masomo ya awali litapewa kipaumbele bila mashaka ya aina yoyote.