Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 3 Sitting 22 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 189 2016-05-18

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. PASCAL Y. HAONGA (K.n.y. MHE. FRANK G. MWAKAJOKA) aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya Zimamoto katika Mpaka wa Tunduma ili kuokoa mali za wafanyabiashara wanaosubiri kuvuka pindi ajali ya moto inapotokea?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Frank George Mwakajoka, Mbunge wa Tunduma, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji katika Halmashauri ya Mji wa Tunduma lina kituo katika eneo la Mtaa wa Kilimanjaro, Wilaya ya Momba katika Mkoa wa Songwe kinachohudumia Wilaya zote ukiwemo mpaka wa Tunduma. Kwa sasa kituo hiki kina gari moja lililopo matengenezoni Mjini Mbeya. Hata hivyo, Askari wanaendelea kutoa Elimu ya Kinga na Tahadhari ya Majanga ya Moto na Utumiaji wa Vifaa kwa Huduma za Kwanza, sambamba na ukaguzi wa majengo na kutoa ushauri kwa wakandarasi na makampuni ya ujenzi kuhusu ujenzi bora wa miundombinu yenye usalama kwa umma.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni azma ya Serikali kupeleka huduma ya zimamoto katika maeneo yote nchini ikiwemo Tunduma. Hata hivyo azma hii nzuri inategemea sana upatikanaji wa rasilimali fedha. Serikali itaendelea kusogeza huduma za zimamoto na uokoaji katika maeneo mbalimbali nchini karibu na wananchi kadri hali ya upatikanaji fedha itakavyoruhusu.