Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Pascal Yohana Haonga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. PASCAL Y. HAONGA (K.n.y. MHE. FRANK G. MWAKAJOKA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya Zimamoto katika Mpaka wa Tunduma ili kuokoa mali za wafanyabiashara wanaosubiri kuvuka pindi ajali ya moto inapotokea?

Supplementary Question 1

MHE. PASCAL Y. HAONGA: Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na kutokuwepo kwa gari ya zimamoto Tunduma, kumeleta madhara makubwa sana kwa wakazi wa Tunduma. Kwa mfano, siku za hivi karibuni kumetokea suala la moto ambalo liliteketeza karibu maduka 500. Hali hii kwa kweli imesababisha wafanyabiashara wengi na wajasiriamali, hali yao kuwa mbaya sana, mitaji yao imepotea. Je, kwa kuwa Serikali leo hii kipaumbele chake ni kununua magari ya washawasha badala ya kununua magari ya zimamoto, iko tayari sasa kuwafidia wale wananchi ambao maduka yao yaliungua kwa sababu ya uzembe wa Serikali? (Makofi)
Swali la pili, kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi kuna tatizo pia kubwa ambalo maaskari wetu pale hawana nyumba na nyingine ambazo nyingi zimejengwa kipindi cha Ukoloni na nyumba nyingi zina nyufa na kituo chenyewe cha Polisi kipo kwenye hali mbaya sana. Je, Serikali itaanza lini ujenzi wa nyumba za maaskari wetu pale Mbozi na Kituo cha Polisi ambacho kwa kweli kimejengwa tangu kipindi cha ukoloni?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la Magari ya washawasha nimelizungumzwa hapa mara mbili, tatu kwamba tunatarajia kuyatumia magari haya vile vile kwa ajili ya kuzimia moto. Tupo katika huo mpango, mazungumzo yameshaanza kati ya Jeshi la Zimamoto na Jeshi la Magereza. Haya magari machache ambayo nimezungumza juzi, yatasaidia. Kwa hiyo, hoja yako Mheshimiwa Frank Mwakajoka imekuja wakati muafaka kwamba hukupaswa kulaumu badala yake upongeze tu kwamba una tatizo la upungufu wa magari ya kuzimia moto, usilaumu kuhusu magari ya washawasha, upongeze kwamba haya washawasha yatakusaidia vilevile. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini kuhusiana na nyumba za askari nalo hili tumelizungumza katika Bajeti yetu vizuri tu kwamba tuna mpango wa kujenga nyumba 4,316 katika mikoa kwa awamu ya kwanza takribani 16. Kwa hiyo, umesema kwamba eneo lako la Tunduma pia unahitaji. Labda nilichukue hili nione jinsi gani katika mgawanyo ule tunaweza kuzingatia ombi lako pia. Siwezi kukuahidi sasa hivi, lakini nalichukua ombi hili tulifanyie kazi.

Name

Shabani Omari Shekilindi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lushoto

Primary Question

MHE. PASCAL Y. HAONGA (K.n.y. MHE. FRANK G. MWAKAJOKA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka huduma ya Zimamoto katika Mpaka wa Tunduma ili kuokoa mali za wafanyabiashara wanaosubiri kuvuka pindi ajali ya moto inapotokea?

Supplementary Question 2

MHE. SHABANI O. SHEKILINDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kituo cha Polisi Lushoto ndiyo cha kwanza na ndiyo kituo kikongwe Tanzania na sasa hivi kinajengwa upya na kinaishia kwenye mtambaa wa panya na kwenye Bajeti sijaona fungu lolote lililotengwa kwa ajili hiyo.
Je, Serikali ina mpango gani wa kumalizia kituo kile?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tuna matatizo ya uchakavu na upungufu wa Vituo vya Polisi katika maeneo mbalimbali nchini. Kwa hiyo, Kituo cha Lushoto ni kimojawapo katika maeneo ambayo yana changamoto hizo. Niseme tu kwamba kama ambayo nimekuwa nikijibu mara kadhaa hapa, tunafahamu changamoto hizo na tutajitahidi kuzipunguza kwa kadri ambavyo tunaweza kupata fedha za kutosha.
Mheshimiwa Naibu Spika, naamini kabisa, kwa kasi hii ambayo Serikali yetu ya Awamu ya Tano imeanza nayo ya ukusanyaji na udhibiti wa matumizi, basi katika muda wa miaka michache ijayo tunaweza tukapata bajeti ya kutosha kuweza kurekebisha matatizo haya ya Vituo vya Polisi pamoja na makazi ya Polisi.