Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 10 Sitting 2 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 34 2023-02-01

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kusaidia ujenzi wa Chuo Kikuu cha Uvuvi na Usafiri Baharini Lindi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia napenda kujibu swali la Mheshimwa Hamida Mohamed Abdhallah, Mbunge wa Lindi Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuongeza idadi ya vyuo vikuu kulingana na uhitaji na upatikanaji wa rasilimali fedha. Katika Mwaka wa Fedha 2022/2023, Serikali kupitia mradi wa Higher Education for Economic Transformation (HEET) imetenga shilingi bilioni 5.8 kwa ajili ya kuanza ujenzi wa kampasi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam katika Mkoa wa Lindi. Kampasi hiyo itakuwa mahususi kwa ajili ya kozi za Ufugaji wa Nyuki, Kilimo-Uchumi na Biashara, Sayansi na Teknolojia ya Chakula, na Uhandisi Kilimo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam tayari kinatoa kozi za Uvuvi katika Shule Kuu ya Akua na Teknolojia ya Uvuvi - Kunduchi na kozi za Sayansi ya Bahari katika Taasisi ya Sayansi ya Bahari Zanzibar, Serikali itafanya tathmini ili kuona kama kuna uhitaji wa kuongeza kozi za Uvuvi na Usafiri wa Baharini katika kampasi mpya ya Lindi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.