Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2015-2020 Session 2 Sitting 5 Water and Irrigation Ofisi ya Rais TAMISEMI. 49 2016-02-01

Name

Lolesia Jeremia Maselle Bukwimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. LOLESIA J. BUKWIMBA aliuliza:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo la maji katika Jimbo la Busanda katika Halmashauri ya Wilaya ya Geita?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI WA TAMISEMI, UTUMISHI NA UTAWALA BORA alijibu:-
Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lolesia Jeremiah Bukwimba, Mbunge wa Jimbo la Busanda, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ili kutatua tatizo la maji katika Jimbo la Busanda, Serikali katika Bajeti ya Mwaka 2015/2016, imefanikiwa kupeleka shilingi bilioni 1.144 ambazo zinatumika kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa miradi ya maji katika Vijiji vya Luhuha, Nyakagomba, Chankolongo, Kabugozo, Chikobe, Chigunga, Inyala na Katoro, ambayo inaendelea kutekelezwa. Miradi hii ikikamilika itachangia kwa kiwango kikubwa kutatua tatizo la maji linalowakabili wananchi wa Jimbo la Busanda.
Mheshimiwa Spika, Serikali itaendelea kuboresha huduma ya maji katika Jimbo la Busanda na Maeneo mengine nchini kwa kadiri rasilimali fedha zinavyopatikana.