Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 14 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 108 2022-04-28

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: -

Je, Serikali inatumia vigezo gani katika mgawanyo wa Watumishi wapya kwenye Halmashauri hususani walimu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana na kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Isack Mtinga Mbunge wa Jimbo la Iramba Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikiajiri watumishi hususani Walimu kulingana na bajeti iliyotengwa kwa mwaka husika. Baada ya kuajiri walimu hugawanywa kila Halmashauri kwa kuzingatia idadi ya mikondo, kila shule kuwa na Walimu wasiopungua Nane na Uwiano wa Mwanafunzi kwa Mwalimu (Pupil Teacher Ratio) kwa shule za Msingi.

Mheshimiwa Spika, kwa shule za sekondari vigezo vinavyotumika kugawa Walimu ni kubainisha idadi ya wanafunzi wanaosoma somo kwa kila kidato, kukokotoa idadi ya mikondo ya madarasa ya wanafunzi kwa kila kidato (mkondo mmoja kuwa na wanafunzi 40 kuanzia Kidato cha Kwanza hadi cha Nne na wanafunzi 35 kwa Kidato cha Tano na Sita. Kubainisha idadi ya vipindi vinavyotakiwa kufundishwa kwa kila somo kwa kuzingatia maelekezo ya mtaala na ukomo wa vipindi anavyofundisha Mwalimu kwa kila somo. Kadirio la juu mwalimu anatakiwa kufundisha vipindi vya dakika 40, thelathini na kadirio la chini visipungue ishirini na nne.