Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, Serikali inatumia vigezo gani katika mgawanyo wa Watumishi wapya kwenye Halmashauri hususani walimu?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu mazuri sana ya Serikali katika suala la mgawanyo, napenda kumuuliza Mheshimiwa Waziri katika mgawanyo uliopita wa Walimu ajira zilizopita, Halmashauri yangu ya Mkalama ilipata walimu 12 tu ikilinganisha na Halmashauri zingine ambazo zilipata zaidi ya walimu 40.

Je, unatuambia nini katika mgawanyo huu unaokuja kuhusu Halmashauri yangu ya Mkalama kwani tuna upungufu wa Walimu zaidi ya 800 katika Halmashauri yangu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Francis Isack Mtinga Mbunge wa Jimbo la Iramba Mashariki, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tutaendelea kuzingatia vigezo vya kupeleka Walimu ambao watapata nafasi hiyo katika Halmashauri zote nchini kulingana na mahitaji. Tunatambua kwamba changamoto bado ni kubwa na mahitaji ya walimu bado ni makubwa lakini kwenye hizi tutaendelea kutenda haki. Kwa hiyo nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaleta kulingana na idadi na mahitaji ya eneo husika. Kwa hiyo, siyo wote 800 lakini ni wale ambao watatosheleza kwa wakati wa sasa. Ahsante sana.