Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 14 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 109 2022-04-28

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa daraja la juu Mto Semu katika Kijiji cha Mwamanongu Meatu?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana na kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Leah Jeremiah Komanya Mbunge wa Jimbo la Meatu, kama ifuatavyo: -
Mheshimiwa Spika, katika Mwaka wa fedha 2005/ 2006, Serikali kupitia Mfuko wa Barabara ilijenga daraja la chini (drifting) lenye urefu wa mita 100 kwa gharama ya Shilingi Milioni 105 ili kurahisisha mawasiliano katika Kijiji cha Mwamanongu.

Mheshimiwa Spika, TARURA inaendelea na upembuzi yakinifu (Geotechnical Investigation) kwa ajili ya kuanza kazi ya usanifu ili kupata gharama za ujenzi wa daraja la juu katika Mto Semu lililopo katika Kijiji cha Mwamanongu.

Mheshimiwa Spika, baada ya kukamilika kwa usanifu wa Daraja hili, Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa hili daraja.