Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa daraja la juu Mto Semu katika Kijiji cha Mwamanongu Meatu?

Supplementary Question 1

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, ni kweli wiki moja iliyopita tumepokea Milioni 43 kwa ajili ya kuanza kazi zilizoainishwa hapo. Kutokana na umuhimu wa daraja katika mto huo uliosababisha Mheshimiwa Rais Samia Suluhu kuahidi daraja la juu mwaka 2015.

Je, Waziri uko tayari kufika katika Kijiji hicho ukajionea adha inayokata mawasiliano ya Kata Nne na Wilaya?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; Maafisa kutoka Wizara ya Ujenzi walifika kukagua hilo daraja pamoja na barabara. Ninataka kujua Je, ni lini Serikali itaipandisha hadhi hilo daraja kuwa TANROADS ili tuweze kupata fedha za kutosha kuihudumia barabara hiyo kutokana na umuhimu wa kiuchumi wa Wilaya ya Meatu na Mkoa wa Simiyu kwa ujumla?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili madogo ya nyongeza ya Mheshimiwa Leah Jeremiah Komanya Mbunge wa Meatu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, niko tayari nitakwenda katika eneo lake kama alivyoahidi, kwa hiyo nitafika kwenda kujionea hiyo hali halisi anayoizungumza Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Spika, Serikali inapokea maombi yote na tunatambua kwamba kuna maombi mengi sana ambayo Halmashauri na Mikoa kupitia Bodi ya Barabara yameyafikisha kwa ajili ya kupandishwa hadhi. Kwa hiyo, Serikali inaendelea kuyafanyia kazi na mara watakapokuwa wamemaliza kujiridhisha maana yake barabara hizo zitapandishwa hadhi. Kwa hiyo, siyo kwamba Serikali inapuuza ni kwa sababu tunafanya tathmini tunaangalia uwezo wa kifedha ili kazi hiyo inapokamilika maana yake na hizo barabara iweze kutengenezwa kulingana na hiyo hadhi.

Name

Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa daraja la juu Mto Semu katika Kijiji cha Mwamanongu Meatu?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Daraja la Mto Nabili linalounganisha Kata ya Bukindo, Kata Nkilinzia ni muhimu sana kwa mawasiliano ya wananchi wa maeneo haya.

Ni lini Serikali itatupatia pesa kujenga daraja hili?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Joseph Mkundi Mbunge wa Ukerewe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimwondoe tu hofu kwamba tumepokea hiki kilio chake na tutakifanyia kazi, kwanza tutawatuma watu wetu wakafanye tathmini na kuona fedha kiasi gani zinahitajika kwa ajili ya ujenzi wa daraja hili. Ahsante sana.

Name

Benaya Liuka Kapinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi ya Mheshimiwa Rais ya ujenzi wa daraja la juu Mto Semu katika Kijiji cha Mwamanongu Meatu?

Supplementary Question 3

MHE. BENAYA L. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Je, ni lini Serikali itatoa fedha za dharura tayari tulishaandika andiko kwa ajili ya barabara ya Kambarage – Mapera – Litoho - Mgumbo pamoja na Mkongotingisa kwenda Muungano, kwa sababu mvua bado zinanyesha na barabara hizi zinataka kutoweka? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Benaya Kapinga, Mbunge wa Mbinga Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ambayo ameainisha Mheshimiwa Mbunge ambayo ipo katika mpango wa Serikali ninaamini kabisa kwamba tuko katika hatua za mwisho za kutafuta fedha ili kuhakikisha hiyo barabara inafanyiwa kazi. Kwa hiyo, nimwondoe hofu mara tutakapopata hiyo fedha maana yake tutaanza ujenzi. Ahsante.