Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 14 Enviroment Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira na Muungano 110 2022-04-28

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI K. n. y. MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuingia kwenye biashara ya Gesi Joto (Carbon Trading)?

Name

Khamis Hamza Khamis

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Uzini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dokta Charles Stephen Kimei, Mbunge wa Vunjo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, biashara ya gesijoto ilianzishwa chini ya Mkataba wa Kyoto unaozibana nchi zilizoendelea kutekeleza miradi ya kupunguza uzalishashaji wa gesijoto (Clean Development Mechanism – CDM) ili kusaidia nchi zinazoendelea kuleta maendeleo endelevu bila kuchafua mazingira.

Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha kuwa Tanzania inaingia na inanufaika na biashara ya hewa ukaa, Ofisi ya Makamu wa Rais iliandaa Mwongozo wa Taifa wa Biashara ya Hewa Ukaa kwa mwaka 2016. Tanzania inayo miradi mitatu ya biashara ya gesijoto inayotekelezwa nchini. Hadi sasa jumla ya tani 900,000 za gesijoto zimeshauzwa kupitia miradi ya uzingatiaji wa kupunguza gesijoto inayotekelezwa nchini.

Mheshimiwa Spika, aidha, miradi minne ya biashara ya soko hiari ya gesijoto imeelekezwa nchini tangu mwaka 2009 na jumla ya tani 1,456,600 za gesijoto zimepunguzwa na kuuzwa kupitia utaratibu huo.

Mheshimiwa Spika, Ofisi ya Makamu wa Rais inafanya mapitio Mwongozo wa Taifa wa Biashara ya Hewa ya Ukaa ili kuwezesha taifa na wananchi wake kushiriki kikamilifu na kunufaika na biashara hii. Aidha, katika kuboresha ushiriki, Wizara ya Maliasili na Utalii inaandaa mwongozo maalum wa usimamizi wa misitu ambayo itashiriki biashara ya gesijto nchini. Ninakushukuru.