Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 14 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 111 2022-04-28

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itawapatia uraia wananchi 6000 kutoka Burundi waliokamilisha mchakato wa maombi ya uraia katika Jimbo la Ulyankulu?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Rehema Juma Migilla, Mbunge wa Ulyankulu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, wananchi wapato 6,000 kutoka Burundi wamekamilisha mchakato wa maombi ya uraia katika Jimbo la Ulyankulu. Wananchi hao walikuwa watoto wa wakimbizi wa Burundi wapatao 162,156 waliopewa uraia mwaka 2009/2010. Wananchi hao pamoja na watoto wapatao 6,620 waliozaliwa baada ya wazazi wao kuwasilisha maombi ya uraia, waliwasilisha maombi ya uraia Serikalini.

Mheshimiwa Spika, kwa ufupi wananchi hao walikamilisha kujaza ipasavyo fomu za maombi ya uraia na kuziwasilisha Serikalini. Maombi yao yalifanyiwa kazi na kwa sasa yapo katika hatua za maamuzi. Mara maamuzi yatakapofanyika, wananchi hao 6,620 watajulishwa hatma ya maombi yao.