Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawapatia uraia wananchi 6000 kutoka Burundi waliokamilisha mchakato wa maombi ya uraia katika Jimbo la Ulyankulu?

Supplementary Question 1

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Spika, nianze kwanza kuishukuru Serikali kwa kukubali maombi ya hawa raia wangu, lakini swali langu lilitaka ni lini huu mchakato utakamilika na kwenye majibu hawajaonesha. Sambamba na hilo nina maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza; Jimbo langu la Ulyankulu katika hizo Kata tatu asilimia 99 ya mwananchi hao kwa sasa ni raia wa Tanzania. Ikijumlisha raia tajinisi na raia wazawa kabisa wa Tanzania lakini wananchi hawa wanaishi chini ya Sheria Na.9 ya wakimbizi ambayo sheria hii sasa inazuia kufanya shughuli zozote za maendeleo ikiwa sambamba na uwekezaji na kufanya shughuli nzuri za kuleta maendeleo kwa wananchi wetu. Sasa je, kwa sasa Serikali haioni kuna kila sababu ya kufuta hii Sheria Na.9 ambayo inazuia maendeleo na uwekezaji kwa wananchi wetu wakati huo Serikali inakwenda kujipanga kwenye zoezi zima la sensa ili kupanga shughuli za kimaendeleo? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, Waziri amesema kwamba hawa raia 6,620 ni watoto wa raia wa Tanzania, yaani wazazi wao kwa sasa ni raia wa Tanzania halafu watoto ni wakimbizi. Sasa je, kwa sababu mchakato haueleweki utakamilika lini, kwa nini sasa hatuoni haja ya UNHCR kuwahudumia hawa wananchi kwa kuwapatia package inayowapatia wakimbizi kwenye makambi mengine ya wakimbizi? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Migilla, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, la kwanza, kuhusu umuhimu wa kufuta Sheria Na.9 ili waruhusiwe kufanya vitu vya maendeleo kwenye makazi yale nadhani Mheshimiwa asubiri tutakapokamilisha kuwapatia uraia wote then hatua za marekebisho ya sheria husika zitafuata. Lakini kama tunakiri kwamba bado watu wengine hawajapewa uraia itakuwa ngumu sana hilo kulitekeleza.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili, watoto hawa wapate package kutoka UNHCR, hilo tutalizungumza, lakini nadhani Mheshimiwa Mbunge jambo la msingi ilikuwa kuharakisha wapate uraia wao ili wa-enjoy haki nyingine kama raia kuliko hilo la package lakini maadam Mheshimiwa Mbunge ameliuliza hapa, tutafanya mawasiliano na wenzetu wa UNHCR kuona uwezekano wa kuzingatia hili ombi lake. Nashukuru. (Makofi)

Name

Agnesta Lambert Kaiza

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. REHEMA J. MIGILLA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itawapatia uraia wananchi 6000 kutoka Burundi waliokamilisha mchakato wa maombi ya uraia katika Jimbo la Ulyankulu?

Supplementary Question 2

MHE. AGNESTA L. KAIZA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Uraia pacha imekuwa ni kilio cha Watanzania walio wengi. Nini kauli ya Serikali rasmi kuhusiana na jambo hili? Ahsante. (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba nimwombe Mheshimiwa Lambert swali hili ni mahsusi, liwasilishwe ili lifanyiwe utafiti hatimaye liweze kujibiwa ipasavyo hapa Bungeni. (Makofi)