Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 14 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 112 2022-04-28

Name

Soud Mohammed Jumah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Donge

Primary Question

MHE. SOUD MOHAMMED JUMAH aliuliza: -

Je, Serikali inatumia vigezo gani kuanzisha vituo vya polisi katika maeneo ambayo idadi ya watu na vitendo vya uhalifu vinaongezeka?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohammed Jumah Soud, Mbunge wa Donge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, vigezo vinavyotumika kuanzisha vituo vya polisi ni ongezeko la watu, ongezeko la matukio ya uhalifu, umbali kati ya kituo kimoja cha polisi na kingine, uwepo wa miundombinu ya Serikali, shughuli za kibiashara pamoja na maeneo ya kimkakati kwa ajili ya ulinzi na usalama wa nchi, likini pia uwezo wa kibajeti na utayari wa wananchi na mamlaka zao za Serikali za Mitaa.

Mheshimiwa Spika, nia ya uanzishwaji wa kituo cha polisi huwasilishwa kwenye Kamati ya Usalama ya Wilaya. Kikao kikiridhia, hoja hupelekwa kwenye Kamati ya Usalama ya Mkoa, kisha ushauri wao huwasilishwa kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi kwa ajili ya utekelezaji ikiwa ni pamoja na mipango ya ujenzi, kupeleka Askari na vitendea kazi. Nashukuru.