Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 14 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 113 2022-04-28

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: -

Je, Serikali imejipangaje katika kuondoa changamoto ya ucheleweshwaji wa viuatilifu kwa wakulima wa zao la korosho?

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Maimuna Salum Mtanda, Mbunge wa Newala Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kuwa huko nyuma kumekuwa na ucheleweshwaji wa viuatilifu. Katika kuondoa changamoto ya ucheleweshwaji wa pembejeo unaosababishwa na mlolongo mrefu wa manunuzi kutoka kwa mzalishaji hadi kumfikia mkulima, Serikali inasimamia uagizaji wa pembejeo kwa kupitia Kamati ya Pamoja ya Pembejeo inayoundwa na Vyama vya Ushirika ambavyo kimsingi ni wakulima wenyewe. Kutokana na utaratibu huo, jukumu la Serikali ni kufuatilia mchakato huo ili manunuzi yafanyike kwa muda muafaka na pembejeo kuwafikia wakulima kwa wakati.

Mheshimiwa Spika, katika msimu wa 2022/2023 Vyama Vikuu vimeagiza sulphur ya unga tani 25,000, viuatilifu vya maji lita milioni 1.5 pamoja na mabomba ya kupuliza 35,000 kwa ajili ya msimu wa 2022/2023 na hadi kufikia Aprili moja jumla ya tani 1,600 na lita 730,724 tayari zimeshapokelewa na kiasi kilichobaki kinatarajiwa kupokelewa kufikia mwisho wa mwezi Mei.