Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Maimuna Salum Mtanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Newala Vijijini

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje katika kuondoa changamoto ya ucheleweshwaji wa viuatilifu kwa wakulima wa zao la korosho?

Supplementary Question 1

MHE. MAIMUNA S. MTANDA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri, lakini Serikali ilituhakikishia kwamba kwa msimu wa 2022/2023 pembejeo zitafika kwa wakati kwa sababu upuliziaji baadhi ya maeneo huanza mwezi Mei. Kwa takwimu ambazo Mheshimiwa Waziri amezitoa, ukiangalia sulphur imefika tani 1,600, bado tani 23,400 lakini viuatilifu vya maji hadi sasa vimefika lita 730,724 bado lita 770,000. Je, Serikali imejipangaje ili kutokurudi kule ambako mwaka jana tulipata changamoto sana ya upatikanaji wa mapema wa pembejeo hizi?

Mheshimiwa Spika, swali la pili ni kwamba, Taasisi ya TPRA ime-test baadhi ya pembejeo ambazo zimefika na kukuta kuna changamoto ya baadhi ya kutokidhi vigezo na kwamba pembejeo hizo zirudishwe zilikotoka. Je, Serikali inatuambiaje hizo pembejeo hazitarudi kwa mlango mwingine kwenda kwa wakulima? Ahsante.

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Maimuna, Mbunge wa Newala Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu viuatilifu ambavyo vimekuwa na mashaka kwanza nilihakikishie Bunge lako siyo viuatilifu vya msimu wa 2022/2023, bali ni viuatilifu ambavyo vilikuwa procured kwa ajili ya msimu wa 2021/2022 na sasa hivi kama Serikali tulichokifanya, viuatilifu vyote ambavyo vilikuwa vina mashaka juu ya ubora vinakusanywa na kuhifadhiwa katika ghala moja katika Mkoa wa Mtwara chini ya usimamizi wa Serikali. Kwa hiyo nataka nimhakikishe Mheshimiwa Mbunge kwamba viuatilifu hivi havitarudi kwa mlango wa nyuma kwenda kwa wakulima.

Mheshimiwa Spika, kuhusu viuatilifu ambavyo vimeshafika ni ukweli kwamba mwaka jana tulikuwa na tatizo na mwaka jana tenda ilitangazwa mwezi Aprili lakini msimu huu tenda tulizitangaza toka mwezi Januari na mpaka sasa mahitaji ya viuatilifu asilimia 50 ya mahitaji ya viuatilifu vya maji tayari viko Mkoa wa Mtwara na hivi vingine tunatarajia vitafika late tarehe 30 Mei na vitashushwa katika Bandari ya Mtwara.

Kwa hiyo, nataka niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge na niwahakikishie wakulima wa korosho, wote watapata viuatilifu vilivyokuwa allocated kwa wakati bila shaka. Pia mwaka huu tumeongeza idadi ya viuatilifu vya maji ili kumpa mkulima matumizi ya viuatilifu vya maji zaidi kuliko matumizi ya sulphur ambayo kwa utafiti wa TARI Naliendele matumizi ya viuatilifu vya maji ni bora zaidi kuliko sulphur na ndomana mwaka huu tumetoa idadi kubwa ya viuatilifu vya maji. Kwa hiyo nataka nimhakikishie Mbunge na wakulima wa korosho kwamba hatutakuwa na matatizo tuliyo experience mwaka jana.

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje katika kuondoa changamoto ya ucheleweshwaji wa viuatilifu kwa wakulima wa zao la korosho?

Supplementary Question 2

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kumekuwa na changamoto ya upatikanaji wa pembejeo za kilimo wakati wa msimu wa kilimo hususan mbolea. Sasa tunapoelekea msimu wa kilimo, Serikali imejipangaje kupambana na changamoto hiyo? Ahsante.

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, changamoto ya msimu uliopita ya upatikanaji siyo suala la availability, tatizo kubwa lilikuwa ni gharama. Mbolea ilikuwepo ndani ya nchi lakini uwezo wa wananchi kununua ulikuwa ndiyo tatizo kubwa. Nataka tu nimwambie Mheshimiwa Mbunge, maelekezo ya Mheshimiwa Rais yako wazi, msimu wa kilimo unaokuja wa 2022/2023, Serikali sasa hivi tuko kwenye majadiliano ndani ya Serikali ili kuona njia ambayo itapunguza bei ya gharama ya mbolea kwa wakulima ili wakulima waweze kuinunua mbolea na waweze kuitumia kwa wakati.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje katika kuondoa changamoto ya ucheleweshwaji wa viuatilifu kwa wakulima wa zao la korosho?

Supplementary Question 3

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Wakulima wengi ambao wanatumia hivi viuatilifu wanahatari kubwa ya kupata magonjwa yasiyoambukiza ikiwemo kansa, mtindio wa ubongo na mengine kutokana na kutokutumia ipasavyo viuatilifu hivi. Nini mkakati wa Serikali kuhakikisha inawalinda wakulima kiafya katika matumizi haya ya viuatilifu? (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Paresso kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli viuatilifu vikitumika vibaya vinakuwa na madhara kama jambo lolote lile, hata chakula watu wakila vibaya kunakuwa na madhara.

Kwa hiyo tunachokifanya kama Serikali ni kwamba tunatoa mafundisho kupitia Tanzania Plant Health Authority iliyokuwa TPRI huko zamani na baadhi ya mazao sasa hivi tumeanza utaratibu wa ku-train vikundi vya vijana ambavyo vinapewa mafunzo maalum na TPRI na kupewa leseni kwa ajili ya kufanya kazi za kupulizia viuatilifu.

Mheshimiwa Spika, vile vile tumeanza kuwataka wasambazaji wa viuatilifu wanapotengeneza vifungashio watumie lugha ya Kiswahili kutoa maelezo ambayo namna ya mkulima kuchanganya ili iwe rahisi mkulima anaponunua kile kiuatilifu kuweza kufanya kazi ile yeye mwenyewe na kupata mwongozo badala ya kutumia lugha ya Kiingereza ambapo inakuwa ni vigumu kuongoza. Kwa hiyo huo ndiyo utaratibu tumeanza na viuatilifu vyote kuanza sasa vinavyosajiliwa TPRI hata vilivyokwisha sajiliwa na nipitie Bunge lako hili kumwagiza Mkurugenzi Mkuu wa Tanzania Plant Health Authority atekeleze maagizo ya Serikali kwamba viuatilifu vyote vifungashio viandikwe kwa lugha kwa Kiswahili ili mkulima aweze kusoma na kuelewa. (Makofi)

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, Serikali imejipangaje katika kuondoa changamoto ya ucheleweshwaji wa viuatilifu kwa wakulima wa zao la korosho?

Supplementary Question 4

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kumekuwa na tatizo la wakulima kugaiwa kiasi kidogo sana cha viuatilifu ukilinganisha na kile kiasi ambacho kimefika katika maeneo husika.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba wakulima wanapata kile kiasi ambacho wanastahili?

Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Answer

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, hivi tunavyoongea sasa hivi tumeiagiza Bodi yetu ya Korosho, lakini vilevile kwa ajili ya kuweza kupata the light data base ya wakulima na ukubwa wa mashamba yao, tunashirikiana na Halmashauri za Wilaya na Serikali za Mkoa kupitia vyama vyao vya ushirika. Cha kwanza, tunachukua takwimu za uuzaji kupitia vyama vya ushirika ili kumjua mkulima na idadi ya uzalishaji wake.

Mheshimiwa Spika, cha pili, kuanzia msimu wa mwaka 2022/2023 Serikali itatenga fedha kwenye bajeti yetu ya kuzipatia Sekretarieti za Mikoa pamoja na Vyama Vikuu vya Ushirika ili zoezi la usajili wa mashamba ya wakulima na utambuzi wa wakulima liweze kufanyika vizuri ili kujua mahitaji halisi ya pembejeo ambazo wakulima wataigawa.

Kwa hiyo, kuna uwezekano kukaendelea kuwepo kwa changamoto kwa muda, lakini ni jambo ambalo tunalolifanyia kazi. Naamini kwamba ndani ya kipindi cha mwaka mmoja au miwili zoezi la usajili wa utambuzi wa wakulima litakuwa limekamilika na tutaondokana na hili tatizo.