Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 14 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 114 2022-04-28

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: -

Je, mazungumzo ya Serikali na wawekezaji kujenga Kiwanda cha Mbolea Kilwa Masoko kwa kutumia gesi asilia yamefikia wapi?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Ally Mohamed Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa viwanda vya mbolea na namna uzalishaji wa mbolea nchini utakavyoongeza tija kwa wakulima na hatimaye kupata mavuno mengi na viwanda kupata malighafi za kutosha kwa ajili ya kuchakata. Serikali inaendelea na majadiliano na wawekezaji mbalimbali wakiwemo Kampuni ya Dangote, Elsewedy na PolyServe ili kuharakisha uwekezaji wa Kiwanda cha Mbolea Kilwa Masoko.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru.