Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, mazungumzo ya Serikali na wawekezaji kujenga Kiwanda cha Mbolea Kilwa Masoko kwa kutumia gesi asilia yamefikia wapi?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante na naipongeza Serikali kwa majadiliano yanayoendelea kati yake na wawekezaji, japo nasikitika kwamba ni karibu mwaka sasa tangu mazungumzo hayo yameanza. Kwa hiyo, kwa umuhimu wa mahitaji ya mbolea nchini, naomba basi mchakato huu ufanyike kwa haraka ili tutatue tatizo kubwa la wakulima ambao wanakosa pembejeo za mbolea msimu mpaka msimu.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Mheshimiwa Waziri mwaka 2021 kupitia Bunge hili aliahidi kuja Kilwa ili kuona mchakato wa uanzishwaji wa kiwanda hiki, lakini nadhani kutokana na majukumu alishindwa kupata nafasi hiyo. Sasa je, yupo tayari baada au ndani ya Bunge hili wakati mchakato wa majadiliano unaendelea, kufuatana nami kwenda Kilwa Masoko ili kuona maendeleo ya maandalizi ya kiwanda cha mbolea?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, naamini Serikali yetu ni sikivu chini ya Rais wetu Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan, tutaharakisha majadiliano haya ili tuweze kufanikisha uwekezaji huu muhimu mapema.

Mheshimiwa Spika, nikijibu swali la pili, naomba nimwahidi, kwa kweli tangu mwaka 2021 hatujapata nafasi, lakini naamini mwaka huu nitakwenda. Nakushukuru sana.

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY M. KASSINGE aliuliza: - Je, mazungumzo ya Serikali na wawekezaji kujenga Kiwanda cha Mbolea Kilwa Masoko kwa kutumia gesi asilia yamefikia wapi?

Supplementary Question 2

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi.

Mheshimiwa Spika, kama ilivyo kwa Kiwanda cha Mbolea Kilwa, ni sawa kabisa na ilivyo na uhitaji wa Kiwanda cha Mbolea Mtwara, hususan Jimbo la Mtwara Mjini kwa sababu malighafi ipo. Sasa tu nataka kujua, ni lini Serikali itajenga kiwanda hicho kwa sababu kitaongeza ajira na wakati huo huo itawezesha nchi kupata mbolea kwa ajili ya kilimo?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji Viwanda na Biashara, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tunza Malapo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema katika jibu la msingi, Serikali ina nia njema kuhakikisha tunavutia wawekezaji wengi kuwekeza katika viwanda vingi ikiwemo viwanda vya mbolea.

Mheshimiwa Spika, pia hili la Mtwara nalo tunalichukulia kwa umuhimu wake kwamba tutaendelea kutafuta wawekezaji zaidi ili weweze kuwekeza Mtwara na maeneo mengine ambayo yana malighafi kwa ajili ya kuzalisha mbolea. Nakushukuru.