Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 14 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 115 2022-04-28

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha SIDO Wilayani Nyasa?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mhandisi Stella Martin Manyanya, Mbunge wa Nyasa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika Bajeti ya mwaka 2022/2023 Wizara kupitia shirika la kuendeleza viwanda vidogo (SIDO) imetenga jumla ya shilingi milioni 950 kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya mitaa ya viwanda. Kati ya fedha hizo, kiasi cha shilingi milioni 100 ni kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Mafunzo na Uzalishaji cha SIDO Wilayani Nyasa. Hivyo, pindi fedha hizo zitakapopokelewa, ujenzi wa kituo hicho utakamilika. Nakushukuru.