Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Kituo cha SIDO Wilayani Nyasa?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwanza nashukuru kwa majibu yenye matumaini kutoka kwa Mheshimiwa Naibu Waziri. Maswali yangu mawili ya nyongeza ni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, imekuwa ni mtindo kabisa wa Wizara hii kuanzisha majengo na kutokumaliza kwa wakati kwa sababu ya kutokupata mgao unaotakiwa kutoka Serikali Kuu, kwa maana ya Wizara ya Fedha: Je, kwa mwaka huu wa 2022, hiyo shilingi milioni 100 iliyoahidiwa ni kweli itatolewa? Naomba commitment ya Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili ni kwamba, Wilaya ya Nyasa haina kabisa chuo chochote kinachotoa mafunzo kwa sasa hivi ikiwemo haya ya ujasiliaamali: Je, SIDO kwa kuwa jengo bado halijakamilika, mtaweza kwenda kutoa mafunzo hayo angalau kila mwezi mara moja wakati tukiendelea na huo ujenzi?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Stella Martini Manyanya, Mbunge wa Nyasa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kumekuwa na changamoto ya upatikanaji wa fedha kwa maana ya kukamilisha vituo vingi vya mafunzo na uzalishaji ambavyo vimeanzishwa katika wilaya na mikoa mbalimbali. Ni nia ya Serikali na sasa tunaamini tutapata hizo fedha ili kukamilisha kituo hiki na vingine ambavyo bado havijakamilika.

Mheshimiwa Spika, suala la pili, nachukuwa maombi ya Mheshimiwa Eng. Stella Manyanya kwamba tuanze sasa kuona namna ya kuanza kutoa mafunzo ya uzalishaji katika maeneo ambapo kuna wajasiliamali wengi ikiwemo katika Jimbo hili la Nyasa ambapo wajasiliamali hawa watapata mafunzo kupitia SIDO.

Mheshimiwa Spika, nawaagiza SIDO waanze sasa kupitia utaratibu ambao siyo rasmi, badala ya kusubiria majengo, waanze kutumia majengo ambayo Halmashauri zinaweza zikatupa kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wazalishaji katika maeneo yote ikiwemo katika Jimbo la Nyasa.