Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 14 Water and Irrigation Wizara ya Maji 116 2022-04-28

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itapeleka maji ya Ziwa Victoria kwenye Kata 24 zilizopo katika Tarafa tatu Wilayani Kishapu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Boniphace Nyangindu Butondo, Mbunge wa Jimbo la Kishapu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, jukumu la Serikali ni kuhakikisha wananchi katika maeneo ya Mijini na Vijijini wanapata huduma ya uhakika ya maji safi na salama.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/ 2023, kazi itaendelea kuhakikisha Kata 24 za Wilaya ya Kishapu zinapata huduma ya maji safi na salama na kufikia lengo la asilimia 85 ifikapo mwaka 2025.