Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji ya Ziwa Victoria kwenye Kata 24 zilizopo katika Tarafa tatu Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mafupi na mazuri. Pia naipongeza sana Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa namna ambavyo inashughulika na changamoto kubwa ya maji na wananchi wa Jimbo la Kishapu kwa ujumla. Tangu mwezi wa pili tarehe 11 mkataba baina ya Emirates Builders wenye thamani ya Shilingi bilioni 6.5 umesainiwa kwa ajili ya usambazaji wa maji ya Ziwa Victoria katika Kata nne; Kata ya Laghana, Mwamashare, Igaga, na Ngofila.

Swali: Je, Serikali iko tayari kuhakikisha kwamba inatoa ile 20% kama advance payment ili mradi huu uanze kutekelezwa kwa wakati kwa maana Mkandarasi mpaka sasa yuko site?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kuambatana nami kwenda Jimboni kuona changamoto zilizoko katika Jimbo la Kishapu na kuhakikisha kwamba atasukuma kazi hii kwa haraka ili mradi maji yaanze kutoka katika Jimbo la Kishapu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa niaba ya Waziri wa Maji naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Butondo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, advance payment tayari zimeanza kutolewa kwa Wakandarasi wote, naamini Emirates naye atakuwa katika list. Suala la kuambatana naye ni moja ya majukumu yangu, hakuna shaka. Nitafika kuhakikisha mradi unatekelezwa. (Makofi)

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji ya Ziwa Victoria kwenye Kata 24 zilizopo katika Tarafa tatu Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 2

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Mradi wa Maji wa Ziwa Victoria unaotoka Mangu kwenda Ilogi ni mradi uliochukuwa muda mrefu sana kutoka 2016. Mwaka 2021 niliuza swali la msingi juu ya mradi huo wa maji. Waziri akaniambia Juni mwaka 2021 mradi ule ungezinduliwa. Sasa ni lini Serikali itazindua mradi wa maji unaotoka Mangu mpaka Ilogi. (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Iddi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, miradi hii ya Ziwa Victoria tunaendelea kuitekeleza. Ipo katika hatua mbalimbali kwa kila eneo, lakini maji ya Ziwa Victoria yataendelea kutumika vizuri, kuhakikisha huduma ya maji safi na salama itapatikana.

Mheshimiwa Spika, ni hivi karibuni uendelezaji na utekelezaji wa mradi huu unaendelea kufanyiwa kazi.

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji ya Ziwa Victoria kwenye Kata 24 zilizopo katika Tarafa tatu Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 3

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Moja ya vijiji vilivyoathirika na machafuko ya Mto Mara ni pamoja na Kijiji cha Kwiguse, Marasibola na Kyamwame na Serikali iliahidi kupeleka maji mbadala kwenye vijiji hivi ambavyo havitumii maji haya kwa sasa. Nataka nijue Serikali imefikia wapi kwenye mpango huu wa kuhakikisha wale wananchi wanapata maji safi na salama?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nimepokea, tutawasiliana na Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)

Name

Abdallah Jafari Chaurembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbagala

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji ya Ziwa Victoria kwenye Kata 24 zilizopo katika Tarafa tatu Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 4

MHE. ABDALLAH J. CHAUREMBO: Mheshimiwa Spika, nilitaka kujua Serikali ina mpango gani wa kulipatia Jimbo la Mbagala maji safi na salama yenye uhakika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Abdallah Chaurembo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maeneo hayo ya Mheshimiwa Mbunge tayari kuna miradi inayoendelea, ipo kwenye utekelezaji hatua za mwisho. Hivi punde maji safi na salama yataunganishwa katika existing lines ili wingi wa maji uweze kuongezeka kwa wananchi. (Makofi)

Name

Felista Deogratius Njau

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji ya Ziwa Victoria kwenye Kata 24 zilizopo katika Tarafa tatu Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 5

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Katika Jimbo la Kawe Kata ya Wazo, mitaa ya Nyakasangwe, Mivumoni na Salala, miundombinu ya maji kwa maana matenki tayari imeshajengwa. Ni lini sasa Serikali itahakikisha maji yanatoka katika mitaa hiyo ili kuwaletea wananchi wale nafuu?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Felista Njau, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maeneo yote ya Kawe miradi iko mwishoni. Hata jana tu nimemwona Mkuu wa Mkoa akiwa na watendaji wetu wa DAWASA wakifuatilia kule, hivyo miradi iko mwishoni. Muda siyo mrefu maji ya kutosha safi na salama yataanza kutoka.

Name

Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Primary Question

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka maji ya Ziwa Victoria kwenye Kata 24 zilizopo katika Tarafa tatu Wilayani Kishapu?

Supplementary Question 6

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana. Wilaya ya Muleba iko kando kando mwa ya Ziwa Victoria, na tuna mradi wa kuvuta maji kwa ajili ya Kata sita za Wilaya ya Muleba; usanifu umekamilika.

Je, ni lini sasa Serikali itatekeleza huo mradi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali Mheshimiwa Mbunge wa Muleba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mara usanifu wa mradi unapokamilika, tunatarajia tuwe na kipindi kifupi cha mwezi mmoja au miwili kuona sasa tunatumia maandiko ya Mhandisi Mshauri ili mradi uanze kutekelezeka. Hivyo, kwa
sababu usanifu umekamilika, tupo katika utaratibu wa kuona sasa tunapata mkandarasi aje kutekeleza huu mradi.