Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 14 Water and Irrigation Wizara ya Maji 117 2022-04-28

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza: -

Je, mpango wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria kutoka Bunda Mjini kwenda Vijiji 33 vya Tarafa ya Chamriho umefikia hatua gani?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Maji, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Boniface Mwita Getere, Mbunge wa Jimbo la Bunda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imeendelea kuboresha huduma ya maji katika Tarafa ya Chamriho ambapo katika mwaka wa fedha 2021/2022 inatekeleza ujenzi wa miradi mipya mitatu ya KirolerI - Kambubu, Mariwanda na Sanzate pamoja na ukarabati wa mradi wa maji wa Nyang’aranga ambayo itatoa huduma ya maji kwa wananchi wapatao 12,648.

Mheshimiwa Spika, nia ya Serikali ni kuhakikisha Wananchi wa tarafa ya Chamriho wanapata huduma ya maji safi na salama na yenye kutosheleza. Katika kutimiza lengo hilo, taratibu za kumwajiri Mtaalam Mshauri kwa ajili ya kufanya usanifu wa mradi wa maji wa kutoka Ziwa Victoria zinaendelea. Matarajio ni kuanza ujenzi wa mradi katika robo ya pili ya mwaka wa fedha 2022/2023.