Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Boniphace Mwita Getere

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bunda

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza: - Je, mpango wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria kutoka Bunda Mjini kwenda Vijiji 33 vya Tarafa ya Chamriho umefikia hatua gani?

Supplementary Question 1

MHE. BONIPHACE M. GETERE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwanza, nawapongeza Wizara ya Maji, wanafanya kazi vizuri sana; na waendelee kufanya hivyo hivyo.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza. Kwa kuwa huu mradi wa maji wa Ziwa Victoria kutoka Bunda Mjini kwenda Bunda Vijijini ni wa muda mrefu sana na una baraka zote za Waziri wa kwanza na Waziri aliyepo sasa hivi Mama Samia Suluhu Hassan, sasa Wizara ipo tayari kuweka mchakato wa single source ili kumpata mkandarasi wa haraka zaidi wa kutekeleza mradi huu?

Mheshimiwa Spika swali la pili; kwa kuwa tuna miradi kichechefu katika vijiji vya Kata ya Nyamswa; vijiji vya Makongoro A, Makongoro B, na Bukama na Vijiji vya Mgeta na Nyang’aranga; sasa ni lini Waziri atafika eneo hilo kusikiliza kero za wananchi kwenye miradi mibovu ya siku nyingi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili Mheshimiwa Gitere kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kupokea pongezi zake. Niseme, tuendelee kushirikiana. Lengo ni kuona tunafikisha maji safi na salama kwa wananchi na kuwatua akina mama ndoo kichwani.

Mheshimiwa Spika, kuhusu Bunda Mjini kuelekea vijijini kutumia single sources; nimepokea ushauri wa Mheshimiwa Mbunge kwa sababu lazima tuajiri mhandisi mshauri ili aweze kutufanyia upembuzi yakinifu na kutuandalia maandalio ya kazi. Baada ya kumpata Mheshimiwa Mbunge wazo lako tutalifanyia kazi kwa kulipa kipaumbele.

Mheshimiwa Spika, kuhusu miradi chefuchefu, ni lengo la Wizara kuimaliza miradi chefuchefu yote, hivyo kufika kwenye maeneo ambayo bado maji ni tatizo ni moja ya majukumu yangu nikuombe Mheshimiwa Mbunge, mara baada ya Bunge hili la bajeti, mwezi wa saba tutaona namna njema ya kufika maeneo yote ambayo yanamiradi ambayo haifanyi vizuri.

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza: - Je, mpango wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria kutoka Bunda Mjini kwenda Vijiji 33 vya Tarafa ya Chamriho umefikia hatua gani?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na jitihada kubwa za Serikali kusambaza maji vijijini jitihada hizi zinaweza kuwa bure iwapo gharama ya kuunganishiwa maji kwenye nyumba za wananchi hazitashuka. Je, Serikali haioni sasa ni wakati umefika wa kuangalia hizi gharama za kuunganishiwa maji kwa wananchi, especially wananchi wa vijijini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa George Mwenisongole kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, gharama za uunganishi Wizara tunaendelea kuzipunguza kwa kuzisogeza bomba kuu ambalo litambunguza umbali wa kutoka kwenye main line kwenda kwa watumiaji, na tayari kazi hii imeanza katika maeneo mbalimbali. Hivyo, ninatarajia kuwa hata katika jimbo lake pia huduma hii itamfikia.

Name

Kiswaga Boniventura Destery

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Magu

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza: - Je, mpango wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria kutoka Bunda Mjini kwenda Vijiji 33 vya Tarafa ya Chamriho umefikia hatua gani?

Supplementary Question 3

MHE. BONIVENTURA D. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru ni lini Serikali itapeleka maji katika Kata ya Kisesa Bujorwa Bukandwe Bujashi ambazo zina matatizo ya maji?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniventura Kiswaga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maeneo yote ambayo bado miradi haijaanza ama miradi imeanza lakini ipo kwenye utekelezaji tutakavyopata fedha, ndani ya mwaka huu wa fedha na mwaka ujao tutakuja kuendelea na kazi ya usambazaji wa maji.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. BONIPHACE M. GETERE aliuliza: - Je, mpango wa kupeleka maji ya Ziwa Victoria kutoka Bunda Mjini kwenda Vijiji 33 vya Tarafa ya Chamriho umefikia hatua gani?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Mji wa Tarime ilipaswa upate maji kutoka Ziwa Victoria kwenye mradi wa miji 21 na Waziri wakati wa bajeti iliyopita aliahidi hapa kwamba kufikia Septemba utakuwa huo mradi umeshaanza na kuelekea matumaini ya kumalizika, lakini mpaka sasa hivi bado haujaanza. Sasa, ni lini huu mradi wa maji kutoka Ziwa Victoria kwenda mji wa Tarime utakamilika?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Matiko kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni miji 28 siyo miji 21. Miji 28 itaanza kutekelezwa hivi punde kabla ya mwaka huu wa fedha kuisha.