Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 21 Health and Social Welfare Wizara ya Afya 184 2022-05-12

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCY J. SABU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kupunguza vifo vya akina mama wajawazito?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, niruhusu kwa kuwa leo ni siku ya Wauguzi Duniani, nitumie Bunge lako Tukufu kuwashukuru wauguzi wote nchini Tanzania kwa kazi kubwa na nzuri ambayo wanaifanya katika kuwahudumia wagonjwa. Tunafahamu kwamba asilimia 80 ya huduma katika hospitali zinafanywa na wauguzi, na tunatambua kwamba wana mzigo mkubwa. Tutaendelea kuajiri watumishi wauguzi wengi tutaendelea kuboresha mazingira ya kufanya kazi kwa wauguzi wote Tanzania. Tunawaomba watimize wajibu wao kwa kuzingatia viapo vyao ambao ni kuokoa maisha.

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Lucy John Sabu, Mbunge wa Viti Maalum, Vijana, Mkoa wa Simiyu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali inatoa elimu kwa Umma hususan kwa akina mama wajawazito kuhusu viashiria vya hatari kupitia njia mbalimbali ikiwemo vyombo vya habari na wakati wa mahudhurio ya kliniki. Aidha, Serikali inasomesha wataalam mbalimbali wa afya ya uzazi katika ngazi ya ubingwa na inaendelea kuimarisha miundombinu katika vituo vya kutolea huduma za afya na kuhakikisha upatikanaji wa dawa na vifaatiba pamoja na kuhakikisha huduma za mama wajawazito zinatolewa bure.