Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 3 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 38 2023-04-06

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Luhindo hadi Ndondo katika barabara Kuu ya Nyoni hadi Mitomoni Wilayani Nyasa?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Eng. Stella Martin Manyanya, Mbunge wa Nyasa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa fedha 2022/2023 Serikali imetenga kiasi cha shilingi bilioni 1.046 kwa ajili ya matengenezo mbalimbali kwenye barabara ya Nyoni - Liparamba hadi Mitomoni. Tayari Mkandarasi yupo eneo la kazi akiendelea na kazi za matengenezo ambapo katika sehemu korofi zenye miinuko na miteremko mikali anazijenga kwa zege na kuweka makalvati maeneo kadhaa. Kazi hizi zinategemewa kukamilika tarehe 30 Juni, 2023, ahsante.