Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Luhindo hadi Ndondo katika barabara Kuu ya Nyoni hadi Mitomoni Wilayani Nyasa?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Spika ahsante sana, kwanza napenda kushukuru kwa majibu ya mazuri ya Serikali.

Mheshimiwa Spika, kufuatia umuhimu wa barabara hii ya Nyoni – Mitomoni kiuchumi Serikali ina mpango gani wa kuanza kufanya upembuzi yakinifu kwa ajili ya ujenzi kwa kiwango cha lami. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa Waheshimiwa Wabunge wa Mkoa wa Ruvuma wamekuwa wakilia, wakipiga magoti humu Bungeni kufuatia changamoto kubwa ya kuvuka katika Mto Ruvuma ulioko Mitomoni ili kutuunganisha na barabara ya Likwilifusi – Mkenda. Je, Serikali ina mpango gani wa kuanza kujenga daraja hili kufuatia kilio kikubwa cha wananchi hao? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Stella Martin Manyanya Mbunge wa Nyasa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nikweli daraja la Mitomoni ni muhimu sana kwa wananchi wa Jimbo la Nyasa nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari tumeishapata mkandarasi na sasa hivi tuko kwenye hatua za mwisho za manunuzi ili mkandarasi aweze kuanza kazi hiyo kwenye kujenga hilo daraja ambalo litagharimu si chini ya bilioni 22. Kwa hiyo, tupo kwenye hatua za mwisho kabisaa za manunuzi kwahiyo daraja hilo litajengwa.

Mheshimiwa Spika, kuhusu kuifanyia upembuzi yakinifu na usanifu wa kina barabara hiyo, Meneja wa Mkoa wa Ruvuma alishaagizwa aweze kufanya tathmini, kufanya makadirio ya gharama ambazo zinaweza kuwa kwa ajili ya kuifanyia hiyo barabara upembuzi na usanifu wa kina wa hiyo barabara, ahsante.

Name

Innocent Sebba Bilakwate

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyerwa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Luhindo hadi Ndondo katika barabara Kuu ya Nyoni hadi Mitomoni Wilayani Nyasa?

Supplementary Question 2

MHE. INNOCENT S. BILAKWATE: Mheshimiwa Spika, ahsante kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya Omulushaka Kwenda mpaka Mlongo mkandarasi ameshapatikana tangu mwaka jana, lakini mapaka leo mkataba bado haujasainiwa. Tatizo liko wapi ili mkataba uweze kusainiwa na mkandarasi aweze kuanza kazi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Innocent Bilakwate, Mbunge wa Kyerwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Barabara ya Olumushaka kwenda hadi Mlongo tayari mkandarasi alishapatikana, na hatua ambayo imebaki sasa ni hatua ya kusaini mkataba ili mkandarasi aweze kukabidhiwa site; na tutaanza kujenga kilomita 50, ahsante.

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Luhindo hadi Ndondo katika barabara Kuu ya Nyoni hadi Mitomoni Wilayani Nyasa?

Supplementary Question 3

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Spika, ahsante na mimi kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya KIA - Sanya Juu ambayo ilikuwa ni ahadi ya Hayati Mheshimiwa Rais Magufuli?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira tuweze kusoma bajeti yetu. Naamini tutakuwa tumefanya mapendekezo ya nini kifanyike kwenye hii barabara ya KIA - Sanya Juu, ahsante.

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Luhindo hadi Ndondo katika barabara Kuu ya Nyoni hadi Mitomoni Wilayani Nyasa?

Supplementary Question 4

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi. Narabara ya kutoka Nagurukuru, Njenje mpaka Liwale ipo katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi. Je ni lini Serikali itajenga barabara hii kwa kiwango cha lami ambayo inaunganisha Jimbo la Kilwa Kusini, Kilwa Kaskazini pamoja na Liwale?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ally Kassinge, Mbunge wa Kilwa Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabra hii Mheshimiwa Waziri alishaahidi. Aliahidi kwenye kamati lakini pia alimuahidi Mbunge, si tu Ally Kassinge lakini hata Mheshimiwa Kuchauka najua anahitaji sana hii barabara; na jana nimekusikia pia ukiichangia hiyo barabara. Naomba tusubiri bajeti tunayokwenda kuijadili sasa hivi, ahsante.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Luhindo hadi Ndondo katika barabara Kuu ya Nyoni hadi Mitomoni Wilayani Nyasa?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini Serikali itajenga barabra ya kutoka Simbo kwenda Kalia?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mhehsimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Josephine Genzabuke, Mbunge Viti Maalum Mkoa wa Kigoma, kama ifuatavyo: -

Mhehsimiwa Spika, Barabara ya Simbo – Ilagala - Kalia, ipo kwenye mpango wa kujenga kwa kiwango cha lami. Sasa hivi kitakachofanyika ni kwanza kupitia usanifu uliofanyika. Kitu tunachokifanya sasa hivi ni kwanza kulijenga daraja la Malagarasi ili liweze kupitika badala ya kutumia vivuko, na baada ya hapo sasa tunafuta kuijenga hiyo barabra yote kwa kiwango cha lami, ahsante.