Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 7 Public Service Management Ofisi ya Rais (Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora) 82 2023-04-14

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaajiri watumishi wa kada ya ulinzi, upishi na makatibu muhtasi katika shule za sekondari za kata nchini?

Name

Ridhiwani Jakaya Kikwete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chalinze

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi na Utawala Bora, naomba kujibu swali namba 82 lilliloulizwa na Mheshimiwa Zacharia Paulo Issaay, Mbunge wa Mbulu Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali imekuwa ikitoa ajira kila mwaka. Kwa mwaka wa fedha 2022/2023, Serikali imetenga nafasi 201 za Makatibu Muhtasi na tano za Wapishi. Watumishi husika wataajiriwa kabla ya mwisho wa mwaka huu wa fedha. Aidha, kwa katika Kifungu cha 6(1) cha Sura ya 298 cha Sheria ya Utumishi wa Umma, Toleo la 2019, Waajiri mbalimbali zikiwemo Mamlaka za Serikali za Mitaa hutenga bajeti kwa kuzingatia kada na maeneo yote ya vipaumbele ikiwemo Walinzi, Wapishi na Makatibu Muhtasi na kuwapanga katika maeneo yenye uhitaji ikiwemo shule za sekondari za kata nchini.