Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 7 Foreign Affairs and International Cooperation Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki 85 2023-04-14

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: -

Je! Tanzania ina Diaspora wangapi na ni upi mchango wao katika uchumi wa nchi?

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dennis Lazaro Londo, Mbunge wa Mikumi kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kwa mujibu wa taarifa kutoka ofisi zetu za uwakilishi wa Kibalozi, idadi ya diaspora wa Tanzania ni milioni 1.5. Aidha, Wizara inakamilisha mfumo wa kidigitali wa uandikishaji wa diaspora (Diaspora Digital hub), ambao unaotarajiwa kukamilika mwezi Juni, 2023. Mfumo huu utawezesha ukusanyaji endelevu wa takwimu za diaspora.

Mheshimiwa Spika, diaspora huchangia katika maendeleo ya nchi kwa kutuma fedha za kigeni nchini (remittances), kuwekeza, kuleta mitaji, utaalam na teknolojia inayoweza kuchangia kukuza uzalishaji wa mazao, bidhaa na huduma mbalimbali zenye tija kiuchumi. Aidha, diaspora hutangaza fursa za kiuchumi, biashara, utalii na uwekezaji zinazopatikana nchini.

Mheshimiwa Spika, katika kipindi cha kuanzia mwezi Januari hadi Desemba, 2022, diaspora wa Tanzania walituma nchini kiasi cha dola za Marekani bilioni 1.1 sawa na shilingi trilioni 2.6. Vilevile, katika kipindi hicho diaspora walifanya uwekezaji kupitia ununuzi wa nyumba na viwanja wenye thamani ya shilingi bilioni 4.4 na ununuzi wa hisa zenye thamani ya shilingi bilioni 2.5. Ahsante sana.