Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. DENNIS L. LONDO aliuliza: - Je! Tanzania ina Diaspora wangapi na ni upi mchango wao katika uchumi wa nchi?

Supplementary Question 1

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, idadi ya watanzania ambao wako diaspora milioni 1.5 ni sawasawa na idani ya wananchi wote ambao wanaoishi katika Mkoa wa Mtwara. Pia ni zaidi ya wananchi ya wananchi wote ambao wanaishi katika Mkoa wa Pwani, Songwe, Iringa, Lindi, Njombe na Katavi.

(a) Mheshimiwa Spika, kwa ukubwa wa idadi ya wananchi hawa; je, Serikali haioni wakati umefika sasa kushirikiana nao kuwa na uongozi rasmi ambao utakuwa daraja kati ya diaspora na Serikali yetu hapa nyumbani?

(b) Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, Serikali imekiri mchango mkubwa wa diaspora, sasa Serikali haioni kwamba wakati umefika wa kuondoa vikwazo na kulieleza Bunge hili mchakato wa uraia ama hadhi maalum umefikia wapi? Nashukuru. (Makofi)

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dennis Lazaro Londo, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu uongozi Serikali inatambua umuhimu wa kuwa na diaspora ambazo ziko organized katika nchi mbalimbali, kwa kutambua hilo Mabalozi wetu wote katika nchi wanazotuwakilisha ndio Walezi wa Jumuiya hizi za diaspora na wamekuwa wakipata ushirikiano mkubwa sana katika Balozi zetu.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na suala la kuondoa vikwazo, hili ni kweli kwa kutambua mchango mkubwa wa diaspora katika maendeleo ya nchi yetu, tayari Serikali imeamua kutoa hadhi maalum kwa diaspora, hivi sasa Serikali inakamilisha taratibu za kuwapa hadhi maalum na muda si mrefu diaspora watapatiwa hadhi maalum. Ninakushukuru sana. (Makofi)