Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 7 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 86 2023-04-14

Name

Kassim Hassan Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwanakwerekwe

Primary Question

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA K.n.y. MHE. HASSAN HAJI KASSIM aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itaweka utaratibu wa kuwa na kitambulisho kimoja chenye taarifa zote za huduma ndani ya kadi moja?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hassan Haji Kassim, Mbunge wa Jimbo la Mwanakwerekwe, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) inatengeneza vitambulisho vya Taifa kwa kutumia teknolojia ya smart card ambapo kitambulisho kinakuwa na chip inayokiwezesha kutumika kwa matumizi mbalimbali. Kitambulisho hiki kinaweza kutumika kama pochi ya fedha ya kielektroniki (E-Wallet), Atm card kwa ajili ya kutoa fedha kutoka mashine ya ATM, huduma za Bima ya Afya, Kitambulisho cha Mpiga Kura na mengineyo.

Mheshimiwa Spika, Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kupitia NIDA inaendelea kufanya mawasiliano na taasisi nyingine zenye vitambulisho ili kuona uwezekano wa kuoainisha taarifa zilizomo katika vitambulisho tofauti kwa madhumuni ya kuwa na kitambulisho kimoja. Mara muafaka utakapofikia wananchi watajulishwa rasmi lini utaratibu huo utaanza kutekelezwa. Ninashukuru.