Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdulhafar Idrissa Juma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtoni

Primary Question

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA K.n.y. MHE. HASSAN HAJI KASSIM aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaweka utaratibu wa kuwa na kitambulisho kimoja chenye taarifa zote za huduma ndani ya kadi moja?

Supplementary Question 1

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri. Kwa niaba ya Mheshimiwa Kassim sasa mawasiliano haya ya Serikali yatakwisha lini, ikizingatiwa Serikali yote ipo Dodoma, ili mchakato huu uanze kufanya kazi. Ninashukuru.

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abdul-hafar kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba Serikali ipo Dodoma lakini taasisi zenye kutoa vitambulisho siyo zote ziko Dodoma, ambacho tunaweza kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge ni kwamba mazungumzo yanaendelea Wizara itafuatilia na ple ambapo kutakuwa na mkwamo basi ngazi za Wizara tutazungumza kwa sababu imeonekana nia ya Watanzania ni kupunguza idadi ya vitambulisho ambavyo mtu anabeba ili kuwa na kitambulisho kimoja chenye taarifa zote. Ninakushukuru.

Name

Simai Hassan Sadiki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nungwi

Primary Question

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA K.n.y. MHE. HASSAN HAJI KASSIM aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaweka utaratibu wa kuwa na kitambulisho kimoja chenye taarifa zote za huduma ndani ya kadi moja?

Supplementary Question 2

MHE. SIMAI HASSAN SADIKI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, haki ya Kitambulisho cha Mtanzania ni haki ya kila raia wa nchi hii.

Je, Serikali haioni haja ya kuambatanisha kitambulisho cha Mtanzania na cheti cha kuzaliwa mara tu baada ya mtoto kuzaliwa? (Makofi)

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika swali la msingi tumesema umuhimu huo upo lakini kuhusu cheti cha kuzaliwa hili litakuwa la kisheria lazima sheria yetu ya NIDA irekebishwe Sheria ya Kitambulisho cha Taifa kwa sababu sheria ile inatambua mtu anayestahili kupewa kitambulisho ni yule aliyefikisha miaka 18 na kuendelea, lakini anayezaliwa leo anastahili kupata kitambulisho cha kuzaliwa. Kwa hivyo tutajitahidi katika marekebisho hayo kuweza kulijumuisha suala ambalo Mheshimiwa Mbunge amelihoji. Nashukuru.

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA K.n.y. MHE. HASSAN HAJI KASSIM aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaweka utaratibu wa kuwa na kitambulisho kimoja chenye taarifa zote za huduma ndani ya kadi moja?

Supplementary Question 3

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, Serikali haioni haja ya kuondoa matumizi ya Kitambulisho cha Taifa wakati Serikali haijajipanga kuwapa wananchi wake vitambulisho na kuondoa usumbufu unaowapata wananchi wake?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Venant Daud kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hoja anayojaribu kuihoji inatokana tu na changamoto tulizozipata. Jambo linalotia faraja ni kwamba katika bajeti hii tunayoendelea kuitekeleza, Serikali imeweza kutoa fedha zote zaidi ya Bilioni 40 zilizokuwa zinahitajika ili kumlipa Mkandarasi na hatimaye aweze kuzalisha vitambulisho.

Mheshimiwa Spika, nimpe assurance Mheshimiwa Mbunge kwamba mara vitambulisho vitakapozalishwa Watanzania wote ambao walikuwa wako kwenye backlog hawajapata vitambulisho watapata vitambulisho vyao. Ninakushukuru.

Name

Rehema Juma Migilla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ulyankulu

Primary Question

MHE. ABDUL-HAFAR IDRISSA JUMA K.n.y. MHE. HASSAN HAJI KASSIM aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaweka utaratibu wa kuwa na kitambulisho kimoja chenye taarifa zote za huduma ndani ya kadi moja?

Supplementary Question 4

MHE. REHEMA J. MIGILLA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Ulyankulu ambao walipatiwa uraia wana cheti cha NIDA, mara kwa mara wamekuwa wakiambiwa watanyang’anywa vitambulisho vyao vya NIDA.

Je, ni sababu zipi ambazo zinapelekea wananchi hawa kutishiwa kunyang’anywa vitambulisho vyao vya uraia?

Name

Sagini Jumanne Abdallah

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Butiama

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Migilla kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hatuna utaratibu wa kumnyang’anya kitambulisho mtu aliye na sifa za kupata kitambulisho hicho, sasa kama pana mamlaka au Afisa yeyote wa Serikali anawatishia kwamba atawanyang’anya, tuombe tu Mheshimiwa Mbunge atupatie hizo taarifa ili tuweze kuzifuatilia kwa umakini kuona sababu na nini kilizosababisha watishiwe hivyo, lakini utaratibu huo haupo. Ninashukuru. (Makofi)