Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 7 Finance and Planning Wizara ya Fedha na Mipango 88 2023-04-14

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kuondoa kodi kwenye vifaa tiba?

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante, kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mipango, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mariam Nassoro Kisangi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, vifaa tiba, kinga, dawa na vitendanishi ni miongoni mwa bidhaa zenye sifa za kupata msamaha wa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kupitia Jedwali la II la Sheria ya Kodi ya Ongezeko la Thamani Sura 148. Jedwali hilo hufanyiwa maboresho mara kwa mara ili kuhakikisha huduma zitokanazo na bidhaa hizi zinapatikana kwa gharama nafuu, ahsante.