Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kuondoa kodi kwenye vifaa tiba?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niulize maswali madogo ya nyongeza. Kwa kuwa katika Hospitali ya Ocean Road kuna changamoto ya baadhi ya mashine za mionzi kukaa muda mrefu bandarani kutokana na kutokamilika kwa taratibu za kikodi; je, Serikali ina mpango gani wa kuweka utaratibu mzuri wa vifaa tiba hivyo kuondolewa mlolongo wa taratibu hizo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; je, Serikali sasa haioni haja ya kuondoa kodi zote kabisa ya vifaa tiba vyote vya wagonjwa wa kansa, figo na kadhalika ili hospitali nyingi ziweze kutibu hayo magonjwa na kutibu Watanzania walio wengi? (Makofi)

Name

Hamad Hassan Chande

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kojani

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Ritta Kabati, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, utaratibu uliopo sasa ni mzuri, kwani Mheshimiwa Waziri wa Afya akisharidhia tu, basi vifaa hivyo vinapatiwa msamaha wa kodi.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kama nilivyojibu katika jibu langu la msingi, ni kwamba vifaa tiba vyote vikiwa vya kansa, figo na kadhalika vinapatiwa msamaha wa kodi baada ya kupata ridhaa tu ya Mheshimiwa Waziri wa Afya, ahsante.

SPIKA: Kwa hiyo, tutakuwa sahihi kwamba anayechelewesha vifaa ni Wizara ya Afya na siyo Wizara ya Fedha.

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, sisi tukipata tu barua ya Mheshimiwa Waziri wa Afya kuhusu vifaa tiba, basi tunatoa msamaha bila pingamizi yoyote.

SPIKA: Waziri wa Nchi, naona Waziri wa Afya hayupo wala Naibu wake. Huu ndiyo uhalisia? Kwa sababu haya maneno ya Mheshimiwa Mariam Kisangi, maana yake atakuwa kayatowa Ocean Road, wanasubiria vifaa viko bandarini.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU: Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Fedha, naomba suala hili tulichukue, tutalifanyia kazi vizuri Serikalini ili tuwe na majibu ambayo yana uhakika na tuweze kumkabidhi Mheshimiwa Mbunge na kuona tatizo hilo linaweza likahitimishwa namna gani. (Makofi)