Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 7 Works, Transport and Communication Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 89 2023-04-14

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: -

Je, ni lini Barabara ya Kilosa hadi Mikumi itajengwa kwa kiwango cha lami?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS) imeanza kujenga barabara ya Kilosa – Ulaya hadi Mikumi kilometa 77 kwa awamu kulingana na kiasi cha fedha kilichotengwa. Katika mwaka wa fedha 2022/2023 kiasi cha shilingi milioni 1,300.00 zimetengwa. Mkataba wa ujenzi umesainiwa kujenga kipande cha kilometa moja katika eneo la Ulaya, ahsante sana.