Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya Kilosa hadi Mikumi itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika,
ahsante kwa kunipatia nafasi kuuliza swali la nyongeza. Kwanza kabisa nashukuru sana kwa majibu ya Serikali kusikia kuwa barabara ya Mikumi – Kilosa imeanza kufikiriwa na itaanzwa kujengwa, lakini naomba ipewe kipaumbele kwa sababu ni barabara muhimu.

Mheshimiwa Spika, swali langu la kwanza: Kutokana na msongomano wa pale Msamvu, Morogoro Manispaa, naomba kujua barabara ya bypass ni lini itajengwa?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili: Ni lini itajengwa Barabara ya Ubena – Ngerengere mpaka Mvuha kwa kiwango cha lami? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya bypass katika Mji wa Morogoro ni sehemu ya Mpango wa Express Way ambayo itajengwa kutoka Chalinze hadi Morogoro na iko tayari kwenye usanifu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba itatokea Kingorowira – Makunganya hadi Sanganga eneo la Mzumbe. Kwa hiyo, hilo litaondoa changamoto ambayo ipo katika Mji wa Morogoro kwa maana ya msongamano. Kwa hiyo, tayari Serikali imelifanyia kazi na limeingizwa kwenye huo mpango.

Mheshimiwa Spika, swali la pili la barabara ya Ubena – Zomozi kwenda Ngerengere, barabara hii ilitangazwa kwanza kwa awamu kilometa 11.6 lakini haikupata Mkandarasi, imetangazwa tena kuijenga kwa kiwango cha lami, na hivi tunavyoongea sasa hivi, tathmini ya zabuni inaendelea kwa barabara hiyo kwa kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Ezra John Chiwelesa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Biharamulo Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya Kilosa hadi Mikumi itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 2

MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Je, ni lini barabara ya Katoke – Nyamirembe itaanza kujengwa kwa kiwango cha lami, kwani ipo kwenye bajeti ya mwaka huu?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mhandisi Ezra Chiwelesa, Mbunge wa Biharamulo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja tumeitengea bajeti kwa ajili ya kuanza maandalizi kuijenga kwa kiwango cha lami na tuna hakika kwamba hata katika bajeti itakayokuja tumependekeza hiyo barabara ianze kujengwa kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya Kilosa hadi Mikumi itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 3

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Wakati Barabara ya Namtumbo – Songea au Songea – Namtumbo inajengwa, Serikali ilifanya tathmini kwa nyumba zilizokuwa karibu na barabara na kuwalipa fedha wenye nyumba hizo zilizobomolewa, lakini leo hii kumejitokeza nyumba zilizokuwa nyuma ya upanuzi wa barabara hiyo zimeenda kuwekewa X na kutakiwa zivunjwe Namtumbo Mjini.

Je, Serikali inaweza kusitisha zoezi hilo mpaka ije ifanye tathmini, nyumba hizo zisibomolewe? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa, Mbunge wa Namtumbo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nimemwelewa vizuri, baada ya mabadiliko ya sheria, tuliongeza upana wa barabara kutoka meta 45 kwenda 60. Kwa hiyo, kila upande tumeongeza kilometa 7.5 kila upande. Sasa kama suala ni hilo, Serikali inafanya tathmini kwa maeneo yote ili kujua gharama halisi ya wale ambao barabara imewafuata. Kwa sababu walikuwa wamejenga maeneo hayo kisheria, lakini kwa sababu tumeamua tupanue barabara zetu kutokana kuongezeka na kuboresha miundombinu yetu, tunalazimika, na hao watu watalipwa fidia, ahsante. (Makofi)

Name

Shamsia Aziz Mtamba

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya Kilosa hadi Mikumi itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 4

MHE. SHAMSIA A. MTAMBA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipatia fursa hii ili nami niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Je, ni lini sasa Serikali itamaliza kutujengea barabara inayotoka Mayanga kuelekea Mkunwa kwenye Halmashauri yetu ya Wilaya kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shamsia, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja itajengwa kwa kiwango cha lami, na kwa kweli itategemea na upatikanaji wa fedha na kwa kweli sina uhakika kama kwenye bajeti hii imo. Tusubiri hiyo bajeti tuone kama itakuwa ipo kwenye mapendekezo kwa ajili ya kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya Kilosa hadi Mikumi itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini Barabara ya kutoka Uvinza mpaka Kasulu itajengwa kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Josephine Genzabuke, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Kigoma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara aliyoitaja ya Uvinza – Kasulu ni sehemu ya barabara kuu ya kutoka Mpanda – Kasulu hadi Nyakanazi na tayari Serikali imeshaanza kuijenga kipande cha Uvinza kwenda Mpanda, na sasa hivi Serikali inatafuta fedha ili kukamilisha kipande hicho ambacho kimebaki takribani kama kilometa 57. Kwa hiyo, tutaikamilisha yote, na tumefunga upande ule wote kuwa barabara ya lami kutoka Nyakanazi – Mpanda hadi Tunduma, ahsante. (Makofi)

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya Kilosa hadi Mikumi itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 6

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Ni lini sasa Serikali itaanza ujenzi wa barabara ya kutoka Mlowo – Kilyamatundu – Ilemba – Mtowisa hadi Majimoto kwa kiwango cha lami? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bupe Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Rukwa, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara ya kipande cha Mloo hadi Kamsamba imewekwa kwenye mapendekezo ya bajeti. Pia ilikuwa ni ahadi ya Waziri Mkuu, aliaagiza, lakini upande wa Kilyamatundu hadi Muze tumeshaanza barabara hiyo kutoka Ntendwa hadi Muze kwenda Kilyamatundu. Kwa hiyo, barabara hiyo tumeshaianza na ni matumaini yetu kwamba tutaendelea kuikamilisha. Ni barabara ndefu yenye kilometa zisizopungua 300, ahsante.

Name

Bahati Keneth Ndingo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya Kilosa hadi Mikumi itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 7

MHE. BAHATI K. NDINGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya muda mrefu ya kujenga barabara ya kutoka Rujewa – Madibira mpaka Mafinga yenye kilometa 151? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bahati Ndingo, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Mbeya, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, barabara hii ilitengewa fedha kwa ajili ya kuanza kuijenga kwa kiwango cha lami. Tunaamini pia tutaiweka kwenye mapendekezo ili iweze kuanza kwa ajili ya uzalishaji mkubwa sana wa mpunga katika eneo ambalo hii barabara inapita, ahsante. (Makofi)

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, ni lini Barabara ya Kilosa hadi Mikumi itajengwa kwa kiwango cha lami?

Supplementary Question 8

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Barabara ya Kolandoto kwenda Kishapu - Mwangongo yenye kilometa 63 ni barabara ambayo sasa imekuwa kero kubwa kwa wananchi wa Kishapu; na barabara hii iko kwenye Mpango wa Bajeti 2022/2023; na iko kwenye Ilani ya Chama chetu cha Mapinduzi; ni lini sasa barabara hii itaanza kutekelezwa rasmi?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Boniphace Butondo, Mbunge wa Kishapu, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nakubaliana naye, lakini hii barabara ni sehemu ya barabara ndefu ambayo tumeitengea bajeti na atakubaliana nami, kwa ajili ya kuanza maandalizi kuijenga kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, tuna uhakika barabara hii kwa kuwa iko kwenye mpango na pia ni barabara kuu, Serikali itaijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.