Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 7 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 91 2023-04-14

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE.CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: -

Je, lini Serikali itafufua Mradi wa Chumvi Ivuna – Itumbula Momba?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Condester Michael Sichalwe, Mbunge wa Jimbo la Momba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kiwanda cha Chumvi cha Itumbula kilichopo Kata ya Ivuna Wilaya ya Momba kilianzishwa na wananchi ambao wameungana pamoja kutoka Kijiji cha Ivuna na Itumbula ili kuanzisha mradi wa kuzalisha chumvi kwenye bwawa la maji ya chumvi.

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua juhudi na jitihada za Wananchi wa Kijiji cha Itumbula na itahakikisha kuwa kiwanda hicho kinaanza uzalishaji. Serikali imeshatoa Shilingi milioni 120 kwa kuelewa kuwa ni mradi wa kimkakati lakini pia Halmashauri ya Wilaya ya Momba imetoa shilingi milioni 50 ili kusaidia katika kutekeleza mradi huo.

Mheshimiwa Spika, aidha mikakati ya Serikali ni kuhakikisha tunahamasisha wawekezaji wengine kuwekeza katika kiwanda hicho.