Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE.CONDESTER M. SICHALWE aliuliza: - Je, lini Serikali itafufua Mradi wa Chumvi Ivuna – Itumbula Momba?

Supplementary Question 1

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru tena kwa kunipa fursa ya kuweza kuuliza maswali mengine mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ambayo Serikali imetoa, majibu haya hayaendani na uhalisia wa sasa kwa namna ambavyo kiwanda kinaendelea. Haya ni majibu ya zamani kabisa. Pamoja na hivyo ninaomba niongeze maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kutokana na mradi huu ni mradi wa kimkakati, tunauliza ni lini Serikali itaanza kutupatia fedha kuendeleza mradi huu kuliko kuanza kutafuta wawekezaji wa kuanza kuwekeza maana yake tulikuwa tumesha ahidiwa kupewa fedha?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kupitia Wizara ya Madini, Waziri mwenye dhamana husika alipotembelea Momba alisema angetuma wataalamu wake waje kutuandikia andiko na kufanya utafiti ni kwa namna gani tuweze kuzalisha kiwango kingi cha chumvi na tuweze kuongezea fedha. Je, Serikali mmeshapata andiko hili la wataalam ili tuweze kuombea fedha ya ziada kutoka kile kiwango ambacho tulikuwa tumepewa?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA:
Mheshsimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Condester Sichalwe, Mbunge wa Momba kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tunajua changamoto ya kiwanda hiki na tathmini inaonyesha tunahitaji takribani shilingi milioni 535 ili kukamilisha ujenzi au uendelezaji wa kiwanda hicho lakini Waheshimiwa Wabunge tunajua kwamba Serikali haifanyi biashara tunachokifanya ni kuwawezesha kama hii mradi maalum wa wale wananchi ili waweze kuendeleza mradi huo.

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema tunahamasisha pia wawekezaji wengine ambao wanaweza kuingia na kushirikiana nao wananchi ambao wameanzisha mradi huu wa chumvi ili uweze kuwa na faida kwa wananchi. Kwa hiyo, Serikali kimsingi haiwezi kufanya biashara lakini inawawezesha wananchi ili waweze kuendeleza shughuli zao za kiuchumi kupitia mradi huu.

Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili la andiko ambalo linaweza kuonesha umuhimu wa kupata fedha kupitia Wizara ya Madini. Hili tutalifanyia kazi na tutawasiliana na Wizara ya Madini ili tuone tumefikia wapi na kumpa jibu kamili Mheshimiwa Mbunge.